Na Lucy Lyatuu, Dodoma
DIWANI wa Kata ya Majengo mkoani hapa Nicholaus Msemo amewataka wakazi wa eneo hilo kuacha kulalamika bali wafanye kazi kwa bidii bila kuchagua huku wakizingatia nidhamu ya fedha.
Amesema hayo wakati akizungumza na gazeti la Mfanyakazi kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya kata hiyo katila siku 100 baada ya uchaguzi mkuu.
Amesema pamoja na mipango na mikakati ya maendeleo aliyopanga kufanya katika kata hiyo lakini pia ni muhimi kwa wakazi wa eneo hilo kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii ili kujikwamua kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
“Ni muhimu kuacha kulalamika, kwamba kazi hii haifai mara ile ndio imayofaa, ni vyema wananchi kujikita kufanya kazi kwa bidii lakini pia kuwa na nidhamu ya fedha kwa kuitumia katika masuala ya msingi, ” Amesema Msemo na kuongeza kuwa nia yake ni wananchi kupewa elimu ya mikopo na kufanya kazi kwa bidii.

Kuhusu siku 100 baada ya uchaguzi amesema ameondoa kero ya malipo kwa wananchi wake wanapohitaji huduma yoyote kutoka serikali za mitaa ambapo gharama zote atahudumia yeye diwani.
“Ilikuwa ni kero kwa wananchi maana wakati mwingine walipohitaji huduma sio wote waliokuwa na fedha kwa ajili ya kulipia huduma hizo kama kupata barua za utambulisho, ” Amesema Diwani Msemo na kuongeza kuwa hata malipo yanayotakiwa kwa wanafunzi wa madarasa ya mitihani katika Kata hiyo atakuwa akiwajibika yeye.
Amesema katika siku 100 ameweza kukarabati shule ya msingi na sekondari iliyopo katika Kata na kwamba changamoto yaaji taka inaendelea kufanyiwa kazi.

