MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Habari

DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda

Author
By Author
Share
4 Min Read

 

Na Lucy Lyatuu

SERIKALI imeiagiza Taasisi Ya Teknolojia Dares Salaam (DIT) kuandaa taarifa itakayowezesha utekelezwaji wa utaratibu wa kupeleka wanafunzi nje ya nchi ili kujifunza  na kupata ujuzi zaidi.

Waziri wa Elimu  Sayansi Na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema hayo kwenye mahafali ya 19 duru ya kwanza ya DIT, Dar es Salaam  ambapo wanafunzi wamehitimu kozi mbalimbali katika Taasisi hiyo.

Akizungumza, Mkenda amesema taarifa ya DIT inatakiwa ipeleke taarifa hiyo Wizarani ndani ya mwezi huu Desemba ambayo  itasaidia  serikali kujua bajeti inayotakiwa ili wanafunzi wanaosoma kozi mbalimbali katika Taasisi hiyo waweze kwenda kujifunza katika nchi nyingine na  kupata ujuzi  utakaowawezesha kuajirika na kujiajiri katika maeneo mbalimbali.

Habari Picha 10510

Amesema  taarifa hiyo itawezesha Wizara kujua kwenye bajeti ya sasa inayoandaliwa iweze kupunguza matumizi ya maeneo mengine ili kutenga fedha kwa ajili ya kupeleka vijana chini ya mpango  wa masomo kwa ushirikiano na taasisi za nje ujulikanao kama sandwich ili kuwawezesha vijana wa Tanzania kupata elimu na ujuzi zaidi.

Kadhalika amesema Serikali itazungumza na Ubalozi wa China ili kwamba ufadhili wa masomo wanaotoa kwa masomo katika vyuo vya nchini humo uwe chini  ya mpango huo wa Sandwich hususani kwa wanaosomea kozi za uhandisi chuoni hapo.

Habari Picha 10511

Amesema DIT imeingia makubalino na Taasisi za Elimu China kwa ajili ya kupeleka wanafunzi kusoma katika vyuo hivyo yaani Sandwich program ambapo chini ya mpango huo mwanafunzi wa DIT  anapelekwa nchini China kusoma kwa ngazi ya  Diploma na anaporudi nchini anakamilisha taratibu za kupata shahada.

 

“Chini ya mpango wa  Sandwich mwanafunzi wa DIT  anapelekwa nchini China kusoma   Diploma na anaporudi nchini anakamilisha taratibu za degree na kwamba mfumo huo unawezesha kuwa na ujuzi wa kufanya kazi katika kampuni mbalimbali za ndani na nje ya nchi,”amesema Mkenda.

 

Amesema wanafunzi wote wanaosomea uhandisi  katika taasisi hiyo wapite katika mfumo huo wa sandwich ili vijana wapate ajira katika maeneo mbalimbali.

 

Aidha amesema katika kuboresha elimu nchini Wizara itatenga fedha chini ya utaratibu wa Samia Scholarship jambo litakalosaidia kutekeleza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kutoa elimu ujuzi ili vijana  wapate ajira ndani na nje.

Habari Picha 10512

 

“Leteni taarifa kwenye bajeti ili mwanafumzi aende huko kunatakiwa nini ili fursa hizo ziwabebe wanafunzi hawa, ”  Amesema.

 

Profesa Mkenda amewaambia wahitimu hao kuwa  elimu haina mwisho, na wasijifungie ndani bali wajifunze kutoka kwa wengine  nakuona kile wanachofanya ili waweze kufanya kazi kwa  kwa ubora na kuongeza ujuzi zaidi.

 

Amesema katika utaratibu huo wa kupeleka wanafunzi nje ya nchi kujifunza wanafunzi  waliomaliza kidato cha sita kuanzia mwakani 2026 wataanza kupelekwa nje kujifunza zaidi.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya DIT, Dkt Richard Masika amewaambiwa wahitimu hao kuwa elimu bila matendo ni sawa na mti bila matunda na kwamba watumie ujuzi walioupata kitoa huduma yenye maudhui ya kitaalam.

 

Amewataka kujua kuwa ulimwengu unahitaji wabunifu na kuwasihi kuongeza bidii, nidhamu na ubunifu zaidi.

 

Mkuu wa DIT, Profesa Preksedis Ndomba amesema Katika kuhakikisha wanafunzi na waalimu wanapata fursa ya kuongeza ujuzi na kubadilishana uzoefu na taasisi nyingine ndani na nje ya nchi taasisi ina makubaliano ya kushirikiana na taasisi zipatazo 50.

Habari Picha 10513

 

Amesema Makubaliano haya yana manufaa makubwa kwa Taasisi  kwani wanafunzi  wananufaika nayo.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

You Might Also Like

Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu

CHAUMMA Yataka Kuvunja Bodi ya Korosho, Kuunda Mamlaka Mpya ya Mazao ya Kimkakati

Fema Mining & Drilling Mfano wa Kuigwa – Musukuma

Kongamano  La Kimataifa La Jotoardhi Laanza Kwa Mafanikio

TFS Yawataka Wananchi Kufuga Nyuki Kuzuia Uharibifu Wa Mazingira

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Msama Aipongeza Hotuba Ya Samia, Atoa Neno Kwa Vijana, Wazee, Wanaharakati
Next Article Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Habari May 24, 2026
Wizara Ya Viwanda Kutekeleza Vipaumbele Saba, Ipo  Miradi Ya Viwanda Ya  Kimkakati
Habari May 22, 2026
Biashara 15 Hazitakiwi Kufanywa Na Wageni Ndani Ya Nchi
Habari May 22, 2026
Wadau wataka mifumo jumuishi kupunguza mzigo wa malezi kwa wenye ulemavu
Habari May 21, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?