MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Chatanda Ampongeza Samia, Aahidi Kuinua Wanawake Kiuchumi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Chatanda Ampongeza Samia, Aahidi Kuinua Wanawake Kiuchumi
Habari

Chatanda Ampongeza Samia, Aahidi Kuinua Wanawake Kiuchumi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE mteule wa Viti Maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa ushindi mkubwa wa kura asilimia 97.6, akisema matokeo hayo yanaashiria imani kubwa ambayo Watanzania wanayo kwake kutokana na kazi kubwa alizozifanya katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
Chatanda amesema UWT, kwa niaba ya wanawake wote nchini, inampongeza Rais Samia kwa mafanikio hayo na inaahidi kushirikiana naye katika kutekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2025–2030, ili kuhakikisha ahadi zote zilizotolewa kwa wananchi, hasa wanawake, zinatimia.
Habari Picha 10241
“Kama mbunge mteule wa viti maalum, nipo tayari kuisimamia utekelezaji wa ilani ya chama chetu. Tutahakikisha tunafuatilia utekelezaji wake ili wananchi, hususan wanawake, wanufaike na maendeleo yaliyopangwa,” amesema Chatanda.
Ameongeza kuwa UWT itakuwa karibu na wanawake katika ngazi zote, kusikiliza kero na changamoto zao, zikiwemo ukatili wa kijinsia na changamoto za kiuchumi, ili hatua madhubuti zichukuliwe kupitia Bunge na Serikali.
Kuhusu uwezeshaji wa wanawake, Chatanda amesisitiza kuwa Rais ameonyesha dhamira ya dhati ya kuinua uchumi wa wananchi kwa kutenga Sh. Bilioni 200 ndani ya siku 100 za kwanza za uongozi wake, kwa ajili ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wakiwemo wanawake.
“Tutahakikisha wanawake wanapata mikopo ya asilimia 10 kutoka halmashauri zetu na kwamba fedha hizo zinatumika ipasavyo. Hatuishii kutoa mikopo tu; tutahakikisha akinamama wanapewa elimu na mafunzo ya matumizi bora ya fedha hizo, ili ziweze kuwanufaisha na kuwainua kiuchumi,” amesema.
Chatanda amesisitiza kuwa jukumu kubwa la UWT ni kuhakikisha kila mwanamke anapata fursa ya kujikomboa kiuchumi kupitia elimu, uwezeshaji na ufuatiliaji wa sera za maendeleo zinazogusa maisha yao.

You Might Also Like

Dkt. Biteko ashiriki kilele cha miaka 60 JWTZ

TRAWU Kupambania Mkataba Wa Hali Bora Kwa Wafanyakazi

Lukuvi Asema 2024 Bangi Ilivunja Rekodi, Tani Zaidi Ya 2000 Zilikamatwa

Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma

VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Watumishi Wa Afya Waliofadhiliwa Watakiwa Kukamilisha Taratibu Ifikapo Novemba 22,2025
Next Article Rita Kabati Aahidi Kuimarisha Miundombinu, Kuwatumikia Wananchi Wa Kilolo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?