MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Profesa Ndunguru: Teknolojia ya Vinasaba Yafungua Ukurasa Mpya Katika Kilimo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Profesa Ndunguru: Teknolojia ya Vinasaba Yafungua Ukurasa Mpya Katika Kilimo
Habari

Profesa Ndunguru: Teknolojia ya Vinasaba Yafungua Ukurasa Mpya Katika Kilimo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
IRINGA: MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imeanza kutumia teknolojia ya utambuzi wa visumbufu kwa njia ya vinasaba (DNA) ili kudhibiti uharibifu wa mazao mashambani, katika eneo la Ruaha Mbuyuni, wilayani Kilolo mkoa wa Iringa.
Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea wakulima wa eneo hilo, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Profesa Joseph Ndunguru, amesema kwa muda mrefu wakulima wamekuwa wakipoteza mazao yao kutokana na mashambulizi ya magonjwa na wadudu waharibifu, hali ambayo imewaathiri kiuchumi na kijamii.
Habari Picha 9927
“Wakulima walikuwa wakitumia viuatilifu bila uhakika wa aina ya visumbufu vinavyoshambulia mimea yao. Hii ilisababisha kutumia dawa zisizo sahihi na kupoteza fedha bila mafanikio,” amesema.
Ameeleza kuwa kwa kutumia teknolojia ya DNA, TPHPA imeweza kutambua aina mbili za bakteria zinazoshambulia zao la vitunguu, na kusababisha mizizi kuoza na mimea kunyauka kabla ya kuvunwa.
“Sasa tumetambua visumbufu husika, na tumeleta viuatilifu vinavyolenga bakteria waliogunduliwa. Hii itasaidia kudhibiti tatizo kwa ufanisi na kuongeza tija kwa wakulima,” amesema.
Habari Picha 9928
Kwa upande wake, mkulima, Jane John, amesema ujio wa teknolojia hiyo utasaidia kuongeza uzalishaji, kwani hapo awali mimea ilikuwa ikishambuliwa bila wao kujua chanzo cha tatizo.
“Mboga mboga zilikuwa zikishambuliwa, majani yanakuwa ya njano, hazivutii na hatuwezi kuuza. Lakini sasa tumepata matumaini ya mavuno bora na sokoni tutakuwa na ushindani,” amesema.
Habari Picha 9929
Hatua hii ni sehemu ya jitihada za serikali kuhamasisha matumizi ya sayansi na teknolojia katika sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi pamoja na visumbufu vya mimea.
Habari Picha 9930

You Might Also Like

Takukuru Kinondoni Yapokea Malalamiko 46 Kuhusu Rushwa

TSB Yatangaza Fursa Za Kilimo, Uwekezaji Wa Mkonge

Dodoma Yang’ara Katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani

Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu yaita wawekezaji

Sera mpya ya viwanda kuzinduliwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mwalim: Nitarudisha Hadhi ya Dar es Salaam Kama Jiji Kamili
Next Article Mafunzo ya Ufundi Sasa Kupatikana Popote Kupitia Programu ya VSOMO”
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yatoa Mwelekeo Maandalizi AFCON 2027, Yaimarisha Miundombinu Nchini
Habari April 17, 2026
Makampuni 100 kushiriki maonesho ya OSHA Njombe
Habari April 17, 2026
Ufaulu  Wa   Somo La Hisabati  Shida Ya Taifa- Wanu
Habari April 16, 2026
Ofisi ya Rais Mipango Yaomba Bilioni 144.85 kwa Bajeti 2026/27
Habari April 16, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?