MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TARI Yawaalika Wakulima Kujifunza Teknolojia Bora 88 Mkoani Morogoro
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TARI Yawaalika Wakulima Kujifunza Teknolojia Bora 88 Mkoani Morogoro
Habari

TARI Yawaalika Wakulima Kujifunza Teknolojia Bora 88 Mkoani Morogoro

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: WAKULIMA pamoja na wadau wa kilimo nchini wamealikwa kutembelea Maonesho ya Wakulima yajulikanayo kama Nanenane ili kupata maarifa na teknolojia bora za kilimo.
Akizungumza katika Maonesho ya Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mkurugenzi wa Kituo cha TARI Ilonga kilichopo Kilosa mkoani Morogoro, Dkt. Arnold Mushongi amesema maonesho hayo ni fursa muhimu kwa wakulima kupata ujuzi wa kisasa.
Amesema mbali na maonesho ya Nanenane, TARI imeweka wataalam wawili pamoja na watumishi watatu watakaokuwepo kwa muda wa mwaka mzima ili kutoa huduma kwa wakulima.
Katika eneo hilo la maonesho, TARI imepanda mazao yote yanayostawi vizuri katika Kanda ya Mashariki na maeneo mengine ya nchi.
“Kuna teknolojia ya mbegu bora, teknolojia za agronomia, teknolojia za udhibiti wa visumbufu, pamoja na teknolojia za kilimo biashara, masoko, baada ya mavuno na kuongeza thamani ya mazao kupitia usindikaji,” amesema.
Dkt. Mushongi ameongeza kuwa shughuli hizo haziendeshwi na TARI peke yake, bali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kutoka kwenye miradi ya wafadhili na vikundi vya wakulima.
“Vipando vya mazao ya nafaka, mikunde, mizizi, mazao ya kibiashara kama miwa na mkonge, pamoja na kilimo misitu, migomba na pamba vyote vimepandwa ili kumwonyesha mkulima na mdau wa mnyororo wa thamani,” amesema.
Pia amesema katika uwanja huo TARI imeweka miundombinu ya umwagiliaji maji wakati wote wa mwaka, “Itachangia kuwa Hub ya uhaulishaji teknolojia na mafunzo muda wote wa mwaka,”.
Amesisitiza kuwa TARI imepewa jukumu kubwa la kufanya, kusimamia, kuratibu na kuendesha tafiti mbalimbali zinazolenga kuboresha kilimo nchini.
Kanda ya Mashariki inahusisha mikoa minne ambayo ni Morogoro, Pwani, Dar es Salaam na Tanga.

You Might Also Like

PSSSF MSHINDI WA KWANZA TUZO ZA UANDAAJI BORA MAHESABU ZA NBAA, 2023

Shilingi bilioni 4.6 kupeleka umeme maeneo ya migodi

Dkt  Biteko ashiriki  Kikao Cha Mawaziri  wa Nishati  Uganda

WMA Yajivunia Kuongezeka Kwa Wafanyakzai

Bahari  Ina Fursa Nyingi Zisizofahamika-Tasac

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article CMSA Yatoa Elimu ya Uwekezaji kwa Wananchi na Wakulima Nanenane
Next Article TARI Yaja Na Jawabu 88 Juu Ya Tindikali, Chumvi Kwenye Udongo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari August 6, 2025
Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?