MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Vijana Ni Chachu Ya Maendeleo Endelevu Wakiwezeshwa-Kikwete
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Vijana Ni Chachu Ya Maendeleo Endelevu Wakiwezeshwa-Kikwete
Habari

Vijana Ni Chachu Ya Maendeleo Endelevu Wakiwezeshwa-Kikwete

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu ) Ridhiwani Kikwete amesema vijana ni chachu ya maendeleo endelevu wakiwezeshwa na kuwajibishwa kimazingira.

Amesema hayo alipokuwa akihutubia mkutano wa Vijana Wa Dunia katika Mji wa Suzhou, China.

Mkutano huo ambao hukutanisha vijana kutoka nchi mbalimbali duniani wakiwemo wanaotoka asasi za kiraia, mashirika ya kitaifa na kimataifa,na serikali mbalimbali ulibeba ujumbe unaosema Vijana ni Chachu ya Maendeleo Endelevu wapewe nafasi kuonyesha Uwepo wao.

 

Washiriki wa mkutano huo wametengeneza maazimio ambayo kila nchi iliyoshiriki itapaswa kuyaangalia ili kunyanyua ustawi wa vijana katika kushiriki ujenzi wa mataifa.

Mkutano huo ambao ulilenga pia kuangalia mafanikio yaliyofikiwa katika utekelezaji wa Malengo ya Millenia kwa upande wa vijana ulihudhuria na kuhutubia kwa njia ya mtandao moja kwa moja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Gilbert Houngbo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Idadi Ya watu duniani-(UNFPA) China  Nadia Rasheed.

Kwa Pamoja washiriki hao walitoa msukumo kwa serikali na wadau wa maendeleo kuhakikisha wanatoa nafasi za kuwasikiliza na kuwahamasisha vijana kushiriki katika ujenzi wa sekta za maendeleo na kuwa wamoja katika kuyafikia malengo yao yakiwemo yale yanayowawezesha kuendelea.

Akihutubia Mkutano huo, Waziri Kikwete ameweka wazi hatua mbalimbali ambazo zimefikiwa na serikali ya Awamu ya Sita ya  Tanzania katika kuwawezesha vijana ikiwemo msisitizo mkubwa uliowekwa Kisera, kisheria na mipango mbalimbali ya kimaendeleo.

Pia Waziri huyo  ameeleza na kuchambua vizuri hatua mbalimbali za mipango ya maendeleo na ushiriki wa vijana ikiwemo ile ya mgawanyo wa asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri, asilimia 30 za fedha za manunuzi ya umma,mikopo ya uwezeshaji wa umma ikiwemo ya NEEC, BEST.

 

Amesema pia zipo  hatua za kushusha riba kwa wakopaji katika mabenki ya biashara, uundaji wa Sera mpya ya Vijana nchini, Programu za maendeleo kama BBT-Madini, Kilimo, Mifugo ambazo zimeonyesha mafanikio makubwa kwa sasa.

Mkutano huo  ni wa 14 kukutanisha nchi wanachama na unafungua fursa kwa nchi wanachama , kukutana na kupeana uzoefu katika kushughulikia changamoto mbalimbali zinazokabili vijana Duniani.

 

You Might Also Like

Asali inayozalishwa nchini kukidhi ubora wa kimataifa

Waziri wa Vijana akutana na Mwita wa Zanzibar

TEA Yakabidhi Miradi Iliyokamilika Wilayani Mtama, Masasi

VETA kushirikiana na Toyota Tanzania kuboresha mafunzo ya ufundi magari

CCCC Yaandaa Tamasha La Dragon Boat

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ikomba: Aliishi Na Watoto Wiki Sita Akiwafundisha Kabla Ya Mtihani WaTaifa
Next Article Mapinduzi ya Elimu Geita: Wasichana Wamerudi Shule kwa Kasi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Rais Wa CWT Suleiman Ikomba Sasa Ni Daktari
Habari September 13, 2025
Salum Mwalim: Nitarejesha Hadhi ya Kanda ya Ziwa na Kuinua Zao la Pamba
Habari September 12, 2025
TEA Yatathmini Utekelezaji na Kupanga Mwelekeo Mpya Kupitia Baraza la Wafanyakazi
Habari September 12, 2025
Manara: Sitapambana na Wafanyabiashara, Nitawatetea
Habari September 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?