MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Habari

Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri

Author
By Author
Share
3 Min Read

Asisitiza Kuendeleza Safari ya Tumaini kwa Walimu

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mwalimu Suleiman Ikomba, ameeleza kusononeshwa na baadhi ya Maofisa wa Halmashauri kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi, licha ya serikali kuu kutoa maelekezo ya wazi juu ya maslahi ya walimu.

Ameeleza hayo alipozungumza na Mwandishi wa habari hii alipotaka kujua ni nini kinachomsononesha kuhusu waalimu hapa nchini.

Amesema moja ya mambo yaliyomvunjia moyo katika safari yake ya uongozi ni kukutana na walimu waliopaswa kupandishwa madaraja kwa mujibu wa sifa zao, lakini wakaachwa kwa sababu ya uzembe wa maofisa wa utumishi katika ngazi ya halmashauri.

“Tumeona walimu waliokuwa na sifa sawa, waliopaswa kupanda madaraja pamoja, lakini mmoja anapandishwa na mwingine anaachwa.

“Wengine wanazidiwa mshahara kwa zaidi ya laki mbili ilhali wameajiriwa siku moja, wana elimu sawa, na wanatekeleza majukumu sawa. Hali hii ni ya kusikitisha na inawaumiza walimu,” amesema.

Amesema uzembe huo unaofanywa na baadhi ya maofisa ni chanzo kikuu cha malalamiko yasiyopaswa kuwepo, hasa ikizingatiwa kuwa serikali kuu imeonyesha nia thabiti ya kutatua changamoto za walimu kupitia maagizo rasmi yanayopaswa kufanyiwa kazi kwenye halmashauri.

“Maagizo kutoka serikali kuu yalikuwa wazi. Tukiwa pamoja na viongozi wa serikali tulitembelea mkoa kwa mkoa, tukakutana na walimu, tukapokea malalamiko yao. Cha kusikitisha ni kuona baadhi ya halmashauri wakishindwa kutekeleza maagizo hayo. Huu ni uzembe wa mtu mmoja lakini unagharimu maisha ya wengi,” amesema.

Kwa upande mwingine ameelezea kufurahishwa na namna ambayo serikali imekuwa ikishirikiana na CWT katika kuzishughulikia kero za walimu.

“Jambo lililonipa furaha isiyoelezeka ni namna tulivyotembea na serikali mkoa kwa mkoa kupitia kliniki ya walimu, tukisikiliza kero zao, tukitafuta suluhu. Kupokelewa na wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, walimu wakifunguka matatizo yao moja kwa moja hiyo ilikuwa safari ya matumaini,” amesema.

Ameahidi katika kipindi chake cha uongozi wa miaka mitano kutoka mwaka huu 2025 hadi 2030, kwamba atahakikisha CWT inabaki kuwa sauti ya kweli ya walimu wote.

Amesema anataka kuwa kiongozi mtetezi wa haki katika kiwango cha ubora unaostahili.

“Natamani kuwa mtetezi wa walimu, lakini kwa njia inayolinda hadhi ya taaluma yetu. Nimegombea kwa sababu nimeona kuwa kazi nzuri imeanza kufanyika.

“Niko hapa kuwahudumia kwa ukamilifu, na kuhakikisha kazi yetu ya ualimu inabaki kuwa yenye heshima na tija kwa taifa,” amesema.

You Might Also Like

Mfanyakazi Ana Wajibu Kupeleka Taarifa za Madai

Midea Group Yafungua Duka Mlimani City Dar Es Salaam

DKT. Biteko Ashiriki Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia Zanzibar

Aprili 2025 Matokeo Awamu Ya Kwanza, Maoni Dira Ya Taifa Na Maendeleo 2050 Kutolewa

Imarisheni Mkakati Wa Kusimamia Usafi Wa Mazingira-Mhagama

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Next Article Samia Aleta Mapinduzi Arusha
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Samia Aleta Mapinduzi Arusha
Habari July 21, 2025
Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’
Habari July 20, 2025
Tumeleta Utulivu na Huduma kwa Walimu’ – Ikomba
Habari July 20, 2025
Afya Bora Yachochea Ustawi wa Wananchi Kigoma
Habari July 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?