MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: FCC Yapongezwa Kukabili Bidhaa Bandia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > FCC Yapongezwa Kukabili Bidhaa Bandia
Habari

FCC Yapongezwa Kukabili Bidhaa Bandia

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
– Mwenyekiti Mlimuka Atembelea Banda la Sabasaba
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: MWENYEKITI wa Tume ya Ushindani (FCC), Dkt. Aggrey Mlimuka, ameipongeza tume hiyo kwa juhudi madhubuti inazochukua katika kudhibiti bidhaa bandia na kukuza ushindani wa haki sokoni.
Amesema mafanikio hayo ni sehemu ya jitihada za serikali kulinda walaji na kuimarisha mazingira ya biashara nchini.
Dkt. Mlimuka alitoa pongezi hizo alipotembelea  Maonesho ya 49 ya Kibiashara yajulikanayo kama Sabasaba mkoani Dar es Salaam alipotembelea banda la Tume ya Ushindani (FCC).
Banda hilo liko ndani ya eneo la Wizara ya Viwanda na Biashara, mkabala na banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Akizungumza na wafanyakazi wa FCC waliopo kwenye banda hilo, Dkt. Mlimuka amesisitiza umuhimu wa tume hiyo kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya bidhaa bandia na umuhimu wa ushindani wa haki katika ukuaji wa uchumi.
“Tume imekuwa ikifanya kazi nzuri kwa kuhakikisha kwamba bidhaa bandia zinadhibitiwa na ushindani wa haki unalindwa. Hii ni muhimu kwa maendeleo ya viwanda vyetu na ustawi wa mlaji wa kawaida,” amesema.
Amesema Maonesho ya Sabasaba ni jukwaa muhimu kwa taasisi kama FCC kuelimisha wananchi kuhusu majukumu yake na kushirikiana na sekta binafsi katika kuhakikisha soko huru na lenye uwiano wa ushindani.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa FCC, Roberta Feruz, amesema ushiriki wa FCC katika maonesho hayo unaendelea kuleta mafanikio makubwa katika kuelimisha umma kuhusu haki zao kama walaji na wajibu wao katika kusaidia kudhibiti bidhaa haramu sokoni.
 “Tumekuwa tukipokea wananchi wengi wanaokuja kutaka kufahamu namna ya kutambua bidhaa bandia, haki zao wanaponunua bidhaa, na namna ya kutoa taarifa iwapo wana mashaka na bidhaa fulani. Hili linaonyesha mwamko mzuri,” amesema.

You Might Also Like

Lugendo Awataka Wananchi Kujenga Tabia Ya Kufanya Usafi

Ridhiwani Kikwete Akagua Maandalizi ya Kilele Mbio za Mwenge Jijini Mwanza

Ridhiwani Afanya Mazungumzo Na Balozi Wa China Nchini, Mingjian

TPDC na PURA Hakikisheni Watanzania Wananufaika na Rasilimali za Mafuta na Gesi- Salome

Majaliwa Aituza UDSM kwa Kuongoza Eneo La Elimu, Utafiti, Ubunifu Sabasaba 2025

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Manyara Kusambaza Mitungi 16,275 ya Gesi kwa Bei ya Ruzuku
Next Article Pato la Mwananchi Lapanda Tabora
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Dkt. Ikomba wa CWT Aeleza Jinsi Elimu Ilivyobadilisha Taswira ya Tanzania kwa Miaka 64
Habari December 9, 2025
Profesa Ndunguru: Mtafiti Aliyejitoa Kusaidia Dunia Kupata Chakula Cha Baadae
Makala December 9, 2025
Profesa Ndunguru Abainisha Mwelekeo Mpya Wa Mageuzi Ya Kilimo Duniani
Habari December 9, 2025
Serikali Kuanzisha Kituo Maalum Cha Kuwezesha Wawekezaji Vijana
Habari December 8, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?