MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi
Habari

Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi

Author
By Author
Share
2 Min Read
Mwandishi Wetu
KIGOMA: MKUU wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Simon Sirro, amezihimiza halmashauri zote katika Wilaya ya Kasulu kuhakikisha zinatenga maeneo rasmi kwa ajili ya uwekezaji, hatua itakayowawezesha wawekezaji kupata ardhi kwa urahisi bila vikwazo vya kisheria au kiutendaji.
Akizungumza katika mkutano wa kujitambulisha kwa viongozi wa Serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wazee maarufu na wananchi, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Sirro amesema uwekezaji ndio njia muhimu ya kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika mkoa huo.
“Nafahamu wilaya yetu ina fursa nyingi kupitia kilimo cha mazao ya chakula na biashara, pamoja na utalii. Nisisitize tu watendaji kuongeza ubunifu, kuweka mifumo mizuri ya usimamizi, na kushirikiana kwa karibu na wawekezaji wote ili kuongeza pato la wilaya, mkoa na taifa,” amesema.
Kwa kuzingatia jiografia ya mkoa wa Kigoma unaopakana na mataifa yenye changamoto za kiusalama, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watumishi wa umma kutoa elimu ya uraia kwa wananchi, ili kuhakikisha wageni wanaoingia nchini wanaheshimu sheria, kanuni na taratibu zilizopo, kwa lengo la kulinda amani na mshikamano.
Sirro amesisitiza umuhimu wa kuzingatia vipaumbele vya mkoa, hasa katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, utekelezaji wa sera ya matumizi bora ya ardhi, kukuza biashara na uwekezaji, pamoja na kuboresha huduma za jamii kama elimu, afya na upatikanaji wa maji safi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Isaac Mwakisu amesema hali ya usalama katika wilaya hiyo ni ya kuridhisha, huku akisisitiza kuwa maeneo yaliyotengwa kwa wawekezaji tayari yatalindwa kwa gharama yoyote ili kuendeleza mazingira bora ya biashara.
Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini, Joyce Ndalichako ameungana na viongozi hao kwa kusisitiza kuwa utekelezaji wa Ilani ya Chama Tawala umeleta mafanikio makubwa wilayani humo, huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutimiza dira ya maendeleo.

You Might Also Like

Kusiluka aitaka TVLA kuongeza tafiti za chanjo 

Ushirikiano Wa Nchi Za Kiafrika Uthibitike Kwa Vitendo -Dkt. Biteko

Kamati Ya Bunge Ustawi Na Maendeleo Ya Jamii Yaridhishwa Wananchi Wanavyofikiwa

Vipima Ulevi Zaidi Ya 3000 Vyakabidhiwa Polisi Na Latra

Rais Samia Aongoza Waombolezaji Kutoa Heshima Za Mwisho Kwa Mbunge Ndungulile

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Programu Ya Samia Extended Scholarship Yazinduliwa
Next Article Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchengerwa Apongeza Shule Ya Sekondari Kibaha Kwa Ufaulu Wa Hali Ya Juu
Habari July 9, 2025
NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani
Habari July 9, 2025
Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi
Habari July 9, 2025
Vumbi la Nyuki Lapewa Uzito Singida: Latajwa Tiba ya Asili Yenye Virutubisho 99
Habari July 9, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?