MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika
Habari

Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
 BODI ya Bima ya Amana (DIB) imesema  imefanikiwa kulipa jumla ya Sh bilioni 9.07 hadi kufikia Machi 2025 kwa wateja waliokuwa na amana katika benki saba zilizofungwa kutokana na kufilisika.
Hata hivyo imewataka wananchi kutembelea banda la Bodi ya Bima ya Amana katika maonyesho ya Sabasaba ili kupata elimu zaidi kuhusu jinsi wanavyolindwa na mfumo huo wa bima endapo taasisi za kifedha zitakumbwa na matatizo.
Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba,  yanayoendelea Dar es Salaam Mkurugenzi wa DIB  Isack Kihwili amesema kiwango hicho cha malipo kimegusa wastani wa asilimia 75.76 ya jumla ya fidia zote zinazostahili kulipwa.
Alizitaja benki zilizohusika   kuwa ni pamoja na FBME ambayo zaidi ya asilimia 57 ya fidia zake tayari imelipwa, Covenant Bank  asilimia 83.73, Kagera Farmers’ Cooperative Bank asilimia 94.06, Meru Community Bank  asilimia 92.35, Mbinga Community Bank  asilimia 84.66, Njombe Community Bank asilimia 87.26 na Efatha Bank ambayo bado inaendelea kufanyiwa tathmini ya fidia.
Amesema wateja ambao bado hawajalipwa ni wale tu ambao hawajawasilisha madai yao ambapo tunawashauri kuwasilisha nyaraka zao ili waweze kulipwa stahiki zao.
Amesema Bodi hiyo ambayo ilianzishwa rasmi mwaka 1991 na kuanza kazi mwaka 1994 ikiwa chini ya usimamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), sasa inajiendesha yenyewe kwa mafanikio.
Amesema hadi kufikia Desemba 2024, bodi ilikuwa na mtaji wa  sh trilioni 1.3, ikiwa ni matokeo ya kuongezeka kwa taasisi za fedha zinazochangia pamoja na maboresho ya mifumo ya usimamizi.
Amesema Kwa sasa kuna jumla ya wachangiaji 42 ambao ni mabenki yaliyosajiliwa na BoT, na huchangia asilimia 0.15 ya amana kwa mwaka kama michango ya bima.
Ameongeza kuwa kiwango cha juu cha fidia kwa mteja mmoja kilikuwa sh 250,000 lakini kikaongezeka hadi sh  milioni 1.5  kwa mwaka 2010, na kufikia sh milioni 7.5 tangu mwaka 2023.
“Kiasi hiki kinamaanisha kuwa, kwa benki yoyote itakayofungwa kwa sasa, mteja mwenye amana ya shilingi   milioni saba na nusu au chini ya hapo atalipwa fidia kamili mara moja,” amesema na kuongeza kuwa iwapo  mteja ana zaidi ya kiwango hicho  basi Bodi itafuata taratibu nyingine za usimamizi wa mali za benki hiyo kwa mujibu wa sheria za ufilisi,” amesema.
Ameongeza kuwa Kwa mujibu wa takwimu, zaidi ya asilimia 99.24 ya wateja wa benki zote nchini wamekingwa na mfumo huo wa bima ya amana, kiwango ambacho kiko juu ya kiwango cha kimataifa kinachotakiwa cha asilimia 90.
Aidha amesema zipo  changamoto kwa wateja wa benki zilizo na matawi au ushirikiano na taasisi kutoka nje ya nchi kutokana na utofauti wa mifumo ya kisheria na kifedha.
Kihwili aliwataka wananchi kutembelea banda la Bodi ya Bima ya Amana katika maonyesho ya Sabasaba ili kupata elimu zaidi kuhusu jinsi wanavyolindwa na mfumo huu wa bima endapo taasisi za kifedha zitakumbwa na matatizo.

You Might Also Like

Rais Samia atoa zaidi ya bil. 2.1 usimikaji wa mifumo, uendeshaji mashauri ya wafanyakazi

NIT yawapika vijana

Serikali Kupeleka Umeme Maeneo Ya Kimkakati

Kaguo Ataja Mbinu Mpya Ukwepaji Kodi Kwenye Mafuta

Kasulu Yatoa Mafunzo Utumiaji wa Mfumo Wa Kieletroniki Kwa Wakuu wa Divisheni, Vitengo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mfumo wa Usalama Majumbani, Umewakumbuka Wenye Ulemavu
Next Article UDSM Yaja Na Bajaji Inayotumia Maji Na Mafuta
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi
Habari July 3, 2025
Wanufaika wa SDF Waeleza Mafaniko Waliyoyapata
Habari July 3, 2025
VETA Dodoma Waleta Mashine Kurahisishia Upekechuaji Wa Alzeti
Habari July 3, 2025
VETA Shinyanga Waja Na Mafunzo Ya Saluni, Mapambo, Urembo
Habari July 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?