MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TTCL Yaweka Punguzo Kubwa Kwa Vifaa Vya Mobile Kwenye Sabasaba
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TTCL Yaweka Punguzo Kubwa Kwa Vifaa Vya Mobile Kwenye Sabasaba
Habari

TTCL Yaweka Punguzo Kubwa Kwa Vifaa Vya Mobile Kwenye Sabasaba

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
SHIRIKA  la Mawasiliano Tanzania (TTCL),  limesema kupitia msimu wa Maonesho Ya 49 Ya Kimataifa Ya Biashara  maarufu kama sabasaba  limeweka punguzo kubwa kwenye vifaa vya  simu (mobile ) ambavyo ni Router, USB modem, na MIFI  Ili  kuwawezesha wateja kumiliki vifaa hivyo na kufurahia ulimwengu wa kidigitali katika kurahisisha mawasiliano.
Aidha shirika  hilo limeijipambanua kama muunganishaji thabiti Wa mawasiliano likizingatia na usalama wa huduma za kwa wateja.
Akizungumza katika Maonesho hayo yanayoendelea  Dar es Salam Meneja wa Banda la TTCL,  Janeth Maeda, ametoa wito kwa Watanzania  kutembelea banda la TTCL ili kujionea huduma za kibunifu, zinazojibu mahitaji halisi ya sasa ya Taasisi, Mashirika na wananchi wa kawaida.
Maeda amesema Shirika hilo linatumia Maonesho hayo kuuhabarisha umma namna  linavyotekeleza wajibu wake kwa Wananchi likiwa limeaminiwa na serikali na kupewa dhamana ya kusimamia na kuendesha miundombinu ya kimkakati ya serikali ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data Kimtandao (NIDC).
“TTCL ni suluhisho la sasa na la baadaye katika huduma za TEHAMA. Hii ndiyo sababu Serikali imeendelea kutuamini kusimamia miundombinu ya kitaifa yenye umuhimu mkubwa kwa usalama wa Taifa na maendeleo endelevu ya kiuchumi,” amesema Maeda.
Amesema TTCL inatoa huduma kwa Taasisi nyingi za Umma ambazo zimeonesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa majukumu na kuongeza ufanisi katika kuwahudumia wananchi.
Amezitaja taasisi hizo ni pamoja na taasisi za Kifedha, Wizara zote, Taasisi na Mashirika ya kiserikali, Sekta ya madini, sekta zisizo za kiserikali, sekta ya Afya na elimu, sekta ya usafirishaji pamoja na sekta ya utalii.
Maeda ameongeza kuwa kwa kutumia huduma za TTCL kupitia Mkongo wa Taifa, Mawasiliano, huduma za Kuhifadhi Data Kimtandao ndani ya nchi, na usambazaji wa mifumo ya TEHAMA, taasisi hizo zimepiga hatua kubwa katika kuongeza ufanisi, kupunguza gharama za mawasiliano na kuimarisha usalama wa taarifa zao.
“Kupitia teknolojia yetu ya fiber optic, tumeweza kuwahudumia mashirika haya kwa kasi ya kuaminika, jambo ambalo linaongeza tija na usalama katika utendaji wao wa kila siku,” ameongeza Maeda.
Amewaalika washiriki wa Maonesho  Kujionea teknolojia ya mawasiliano ya kisasa inayowezeshwa na mtandao wa TTCL, kujifunza kuhusu namna bora ya kidigitali ya uhifadhi salama wa taarifa (Data Center), na kupata maarifa ya namna ya kupunguza gharama na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

You Might Also Like

Uongozi CHADEMA Kanda Ya Kati Upo Imara

Wananchi Waendelee Kupewe Elimu Kuhusu Bioteknolojia

Ridhiwan Kikwete awaagiza maofisa kazi kushirikiana na WCF

Hivi Ndivyo Vipaumbele Vya Maliasili

Dar es Salaam Kuunda Kamati Ya Kupitia Majengo Chakavu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sanaa, Utamaduni Yaimarisha Urafiki Wa China, Afrika
Next Article Martha Mariki Achukua Fomu Kutetea Nafasi Yake Katavi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Singida Yapokea Zaidi Ya Milioni  Moja 
Habari July 5, 2025
THBUB Mdau Mkubwa Utekelezaji Wa Majukumu 
Habari July 5, 2025
NBS: Utumiaji Wa Takwimu Nyenzo Muhimu Kwa Mama Lishe
Habari July 5, 2025
FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara
Habari July 5, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?