MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yazidi Kuhamasisha Nishati Safi, Yatoa Mitungi 225 Kwa Watumishi Gereza kuu Maweni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yazidi Kuhamasisha Nishati Safi, Yatoa Mitungi 225 Kwa Watumishi Gereza kuu Maweni
Habari

Serikali Yazidi Kuhamasisha Nishati Safi, Yatoa Mitungi 225 Kwa Watumishi Gereza kuu Maweni

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kuwezesha, kuhamasisha na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa watumishi wa magereza na wananchi ili kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia (2024 – 2034).

Hayo yamebainishwa leo  na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB),  Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu wakati wa uzinduzi wa kugawa majiko ya gesi kwa watumishi wa magereza iliyofanyika Gereza Kuu la Maweni jijini Tanga.

“Hii yote ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100 zihame kutoka katika matumizi ya nishati chafu na kuhamia katika nishati safi ya kupikia, ” Ameongeza.

Vile vile ameongeza kuwa, Magereza yote ya mkoa wa Tanga tayari yanatumia makaa ya mawe ya Rafiki Briquette unaozalishwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).

 

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa REA  Hassan Saidy amewataka watumishi wa magereza kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kuhusu matumizi na umuhimu wa nishati safi ya kupikia ili kuifanya nishati hiyo kuwa endelevu, pia ni chachu kwa wananchi katika kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye mkakati wa kitaifa.

Amesema kuwa, gharama ya mradi wote ni zaidi ya shilingi Bilioni 35.2 ambapo Wakala wa Nishati Vijijini unatoa ruzuku ya sh bilioni 26.5 Sawa na asilimia 75.4 ya gharama ili kuwezesha utekelezaji wake.

 

 

Kwa upande wake, ACP Nade Baynit, Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga ameishukuru REA kwa kuwezesha watumishi magereza kutumia nishati safi ya kupikia.

Aidha, amewataka watumishi hao kuchangamkia fursa hiyo inayotolewa na REA kwa watumishi wa magereza kwa kujipatia mtungi wa gesi na majiko ya gesi ya sahani mbili  bure na waeendelee kuwa mabalozi wa nishati hiyo kwa wananchi.

Naye, Mratibu wa nishati safi kutoka kampuni ya Lake Gas Ltd  Ramadhani Siasa amesema watatekeleza mradi huo kwa kuzingatia makubaliano ya Mkataba wa kusambaza mitungi ya gesi ya kupikia pamoja na kutoa elimu, kuhamasisha wananchi ili kuchochea matumizi ya nishati hiyo.

 

 

 

You Might Also Like

BAKITA Lapongeza Sheria Za Tanzania Kuandikwa Kwa Lugha Ya Kiswahili

Apongeza watumishi kwa kutoa huduma bora kwa walimu

GST Yaelezea Mafanikio Yake

Mtafiti UDSM Atafiti Mimea Ya Asili Kudhiti Fangasi Kwenye Mimea

Jeshi la polisi kumhoji anayesambaza taarifa za uongo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article UDSM Chasaini Mikataba Na Kampuni Za Kichina, Kujengea Uzoefu Wanafunzi Wake
Next Article TARURA Dar Yaendelea Na Ujenzi Wa Miundombinu Ya Barabara Iliyosimama Kutokana Na Mvua
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni
Habari July 1, 2025
Msomi Wa Afya, Fatuma Atia Nia Jimbo la Dodoma Mjini
Habari July 1, 2025
Dkt. Mashimba Achukua Fomu Ya Kuwania Nafasi Ya Ubunge
Habari July 1, 2025
TPHPA, MUCE Wasaini Hati Ya Makubaliano Maeneo Yanayogusa Sayansi
Habari July 1, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?