Na Danson Kaijage
DODOMA: NAIBU Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile ameelezea jinsi sekta hiyo inavyogusa maisha ya watanzania kupitia reli, barabara, anga au usafiri wa majini.
Amesema hayo alipotembelea Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka huu 2025, inayofanyika jijini Dodoma.

Amesema kwa umuhimu wa sekta hoyo, inahitajika kuendelea kujenga mfumo unaomuweka mwananchi mbele kwa kuhakikisha huduma ni za haraka, salama, na zenye tija.
Pia amesema maonesho hayo yanaongeza uwazi na uelewa kwa wananchi kuhusu huduma zinazotolewa na Wizara ya Uchukuzi, sambamba na kuwaweka karibu zaidi na Serikali yao.
“Katika wiki hii, tunapaswa kujiuliza kama tunamtumikia mwananchi kwa uadilifu na ufanisi, kwani Watumishi wa umma tuna jukumu la kuakisi maadili ya uwajibikaji, uvumilivu na ubunifu kwa manufaa ya Taifa letu,” amesena.
Akizungumza na watendaji wa wizara hiyo, amesema Wiki ya Utumishi wa Umma ni fursa muhimu ya kujifunza, kusikiliza wananchi, na kuboresha mifumo ya utoaji huduma, hasa katika sekta ya uchukuzi ambayo ndiyo mhimili wa maendeleo ya kiuchumi.