MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wachimbaji Wadogo Wafikiwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wachimbaji Wadogo Wafikiwa
Habari

Wachimbaji Wadogo Wafikiwa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI inaendelea na juhudi za kupunguza mzigo wa tozo kwa Wachimbaji wadogo wa dhahabu hapa nchini kwa kufanya mapitio ya ada na ushuru mbalimbali anazotozwa katika mnyororo wa uchimbaji na uchenjuaji wa madini.
Waziri wa Madini Anthony Mavunde, amesema hayo  Bungeni Jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Busanda, Tumaini Magessa ambaye alitaka kujua ni lini Serikali itapitia upya tozo zilizopo kwenye mnyororo wa uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu zinazowaelemea Wachimbaji Wadogo.
Katika majibu yake, Waziri Mavunde amesema kuwa kupitia Mkakati wa Kuboresha Mazingira ya Biashara, Wizara ya Madini imefanya utafiti wa tozo 66 zinazotozwa na Halmashauri mbalimbali katika shughuli za uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu.
Ametaja tozo hizo kuwa ni ushuru wa karasha, ada ya ukaguzi, kodi ya  thamani, ushuru wa kusafirisha miamba ya madini, na visusi (mabaki ya miamba baada ya uchenjuaji).
“Katika kutatua changamoto hizi, Wizara iliitisha kikao Mwezi Agosti, 2024 Mkoani Singida ambacho kilishirikisha Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Wizara ya Fedha, Tume ya Madini, STAMICO, Halmashauri za Wilaya (Ikungi, Chunya, Kahama, Msalala, Meatu, Shinyanga, Mtama na Lindi),
“FEMATA na TAWOMA. Rasimu ya Mapendekezo ya Maboresho tayari imeshaandaliwa na ipo katika hatua ya kufanyiwa mapitio na tathmini, ambapo Matokeo ya tathmini hiyo yatatusaidia katika kupanga tozo rafiki kwa wachimbaji wadogo,” amesema.
Pia amesema serikali inaendelea na maboresho makubwa ya mfumo wa kodi kupitia Tume ya Maboresho ya Kodi iliyoanzishwa na  Rais Samia Suluhu Hassan, tume hiyo inatarajiwa kutoa mapendekezo yatakayosaidia kupunguza changamoto za kikodi zinazowakabili wachimbaji hao wadogo.
Hatua hizo zinadhihirisha dhamira ya Serikali katika kuboresha mazingira ya uchimbaji mdogo wa madini na kukuza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa nchi.

You Might Also Like

Tume Ya Kurekebisha Sheria Tanzania Kuipitia Sheria Ya Takwimu

Serikali Inatoa Kipaumbele Kufikisha Umeme Taasis Zinazotoa Huduma Kwa Jamii- Kapinga

Kameta awaasa watanzania kutonunuliwa  kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mtaa, Mkuu

Tanzania kujiimarisha zaidi kidiplomasia – Majaliwa

Lukuvi Asema 2024 Bangi Ilivunja Rekodi, Tani Zaidi Ya 2000 Zilikamatwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ushiriki Wa Wanawake, Wasichana Katika Sayansi Ni Mdogo
Next Article Masauni: Mapendekezo Ya Kulifanya NEMC Kuwa Mamlaka Yamepokelewa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?