MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa
Habari

Tumeanza Kufanyia Kazi Maelekezo Ya Rais Samia – Bashungwa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Awajulia Hali Majeruhi 16, Waliopoteza Maisha 11
Na Lucy Ngowi
KAGERA: WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imeanza kufanyia kazi maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanya marekebisho ya kuwa na mfumo wa leseni za udereva ili kuwapunguzia alama madereva wanaofanya makosa yenye kuhatarisha usalama barabarani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema hayo baada ya kufika eneo la Kabukome katika Kata ya Nyarubango wilayani Biharamulo mkoani Kagera, kulipotokea ajali ya basi la abiria lenye namba za usajili T857 DHW.
Pia aliwajulia hali majeruhi wanaoendelea kupewa matibabu katika Hospitali Teule ya Biharamulo, Disemba 21, 2024.
Bashungwa amesema maelekezo hayo ya Rais Samia ni pamoja na kuwafungia leseni madereva wanaofanya makosa yanayohatarisha usalama barabarani.
Basi hilo lililopata ajali lilikuwa linafanya safari kutoka Kigoma kwenda Bukoba wakati liliposimama kushusha abiria ambaye alipitilizwa kwenye kituo, lilishindwa kuondoka na kurudi nyuma kisha kuacha njia na kupinduka.
Ajali hiyo imesababisha vifo vya abiria 11 na majeruhi 16 ambapo majeruhi wanaendelea na matibabu katika  Hospitali Teule ya Biharamulo mkoani Kagera.
Bashungwa ametoa pole kwa  familia, ndugu na jamaa wote walioguswa na ajali hiyo na kutoa wito kwa watanzania kuendelea kuwaombea majeruhi wapone haraka.
Kwa Upande wake, Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo majeruhi waliko, Gresmus Sebuyoya amesema majeruhi 26 wameruhusiwa na wengine 16 wanaendelea na matibabu na ungalizi wa karibu.
“Tumebaki na watoto wanne ambao wanaendelea vizuri, wanaume tunao sita, vifo tulikuwa navyo 11, wanawake watano, wanaume wanne  na watoto wawili” amesema.

You Might Also Like

TUCTA Yaitaka Jamii Kuwapa Nafasi Vijana Wenye Changamoto za Kimwili

Chalamila Asema Serikali Inafanyia Kazi Changamoto, Mradi Wa Mabasi Yaendayo Haraka

Wanafunzi 571 watunukiwa Stashahada Na Astashaha Za Vyuo Vya Polisi

Serikali  Kutumia Fursa  ya AFCON,  Miss World Na IPU Kukuza Utalii Nchini

Baraza la uuguzi na ukunga lawakaribisha wenye malalamiko

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TARI Yawafikia Wakulima Kilosa, Kilimo Shadidi Cha Mpunga
Next Article Mkurugezi Mkuu LATRA, Kamanda Ng’anzi Wafanya Ukaguzi Wa Kushtukiza Stendi Ya Magufuli
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPHPA Kuja Na Ramani Ya Visumbufu Nchi Nzima
Habari August 9, 2026
Dkt. Samia: Ushirika Simamieni Matrekta Kwa Manufaa Ya Wakulima
Habari August 9, 2026
Jeshi La Zimamoto Yaimarisha Elimu Kwa Wananchi Kuhusu Matumizi Salama Ya Nishati Ya Kupikia
Habari August 9, 2026
DC Kondoa  Aipongeza TFS Kwa Teknolojia Ya Uhifadhi Wa Misitu Na Utali
Habari August 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?