MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: OUT Yawapiga Msasa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > OUT Yawapiga Msasa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa
Habari

OUT Yawapiga Msasa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Mwandishi Wetu

DODOMA:CHUO Kikuu Huria Tanzania (OUT), kinaendesha Mafunzo ya Ufuatiliaji na Tathmini kwa watumishi wa mamlaka za serikali za mitaa pamoja tawala za mikoa ili kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa maendeleo ya miradi inayowekezwa na serikali.

Kaimu Mkurugenzi kitengo cha Ufuatiliaji na Tathimini, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI, Mussa Otieno amesema hayo alipomwakilisha Katibu Mkuu Adolf Ndunguru, wakati akifungua mafunzo ya awamu ya pili ya Ufuatiliaji na Tathmini

Amesema mafunzo hayo yanafanyika ili kuwaimarisha watumishi waliopo katika idara hizo kwani wataimarika katika utendaji wao wa kazi.

Amesema serikali inatumia bajeti kubwa katika mamlaka za serikali za mitaa, hivyo anaamini kuwa baada ya mafunzo hayo watumishi hao watakuwa wameimarika.

“Baada ya mafunzo haya mtumishi atakuwa na uwezo wa kutimiza malengo yanayotakiwa katika masuala ya ufuatiliaji na tathmini ili miradi ya serikali iendane na malengo yaliyopangwa.

“Tukatumie vyema utaalam tutaopata hapa na tukawashirikishe na wenzetu tunaofanya nao kazi pamoja, ili kuwa na timu nzuri kwa ajili ya kuimarisha ufuatiliaji na tathmini katika halmashauri tunazotoka,”amesema.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini wa Utendaji wa serikali, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sakina Mwinyimkuu amesema serikali za mitaa ndiyo mtekelezaji mkubwa wa shughuli za serikali karibia asilimia 70 ya shughuli zote zinatekelezwa na mamlaka ya serikali za mitaa.

Hivyo mafunzo hayo kwa washiriki hao yataiongezea uwezo serikali kufikia malengo yake ya kitaifa ikiwemo dira ya maendeleo.

“Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni mdau anayetusaidia kujengea uwezo taasisi za umma katika ufuatiliaji na tathmini, serikali za mitaa ndiyo watekelezaji wa shughuli za serikali na ndiyo wanaotoa picha ya utendaji wa serikali kwa jamii.

“Hili ni eneo linaloweza kuwabadilisha mitizamo ya wananchi na kuwajengea imani kwa serikali yao kwa kuona inasimamia vyema utekelezaji wa sera, miradi na mipango.

‘Hivyo mafunzo haya yatawasidia vyema utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoibuliwa na halmashauri na mingine ya kitaifa inayotekelezwa katika halmashauri,” amesema.

Mratibu wa Mafunzo ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi kutoka OUT, Dkt. Emmanuel Mallya amesema chuo hicho kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, kinaendesha mafunzo hayo ili serikali iweze kushuhudia mabadiliko makubwa ambayo yanalenga kuimarisha utendajikazi hasa katika upande wa ufuatiliaji na tathmini.

Mwenyekiti wa washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni Katibu Tawala msaidizi sehemu ya Usimamizi, Ufutiliaji na Ukaguzi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Pius Ngaiza, ameishukuru serikali kwa kuwapa mafunzo hayo kwa kuwa wengi walikuwa wanafanya tathmini na ufuatiliaji katika namna ambayo ilileta shida hasa katika ukaguzi,.

Amesema mafunzo hayo yamewaimarisha hivyo watafanya kazi kwa kufuata mfumo unaotakiwa kiofisi na hata kitaifa.

Mafunzo haya ni mwendelezo wa mafunzo ya awali yaliyoendeshwa katika jiji la Arusha kanzia Oktoba saba hadi 11, 2024.

Wasiriki 90 kutoka mikoa 13 walishiriki ambapo kiujumla inakuwa asilimia 70 ya halmashauri, manispaa na majiji yote nchini kupata mafunzo hayo ya ufuatiliaji na tathmini.

You Might Also Like

Ridhiwani: Maandalizi Mei Mosi  Yafikia Asilimia 88

Askari Wawili wa JWTZ Wafariki, Wanne Wajeruhiwa DRC

TPHPA Kuipokea Ndege Yake

TRAWU Kupambania Mkataba Wa Hali Bora Kwa Wafanyakazi

Wajumbe IPA Zanzibar Wafanya Ziara TEA

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TARI: Mabadiliko Ya Tabia Nchi Yamepunguza Ufanisi Wa Mbegu
Next Article Kasulu Yatoa Mafunzo Utumiaji wa Mfumo Wa Kieletroniki Kwa Wakuu wa Divisheni, Vitengo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?