MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: REA Yatoa Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi, Shule ya Samia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > REA Yatoa Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi, Shule ya Samia
Habari

REA Yatoa Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi, Shule ya Samia

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu’
WAKALA wa Nishati Vijijini (REA),umetoa sh. Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi ya kupikia katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Samia Suluhu Hassan mkoani Ruvuma.
Shule hiyo ya kisasa yenye wanafunzi zaidi ya 540 iliyopo Wilaya ya Namtumbo katika Mkoa wa Ruvuma imezinduliwa rasmi na Rais Samia Suluhu Hassan Septemba 27, Mwaka huu.
Akizungumza  baada ya uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Mipango na Utafiti REA, Godfrey Chibulunje ameshukuru serikali kwa kutoa fedha zinazowezesha wakala kutekeleza miradi yake mbalimbali kwa wakati ikiwamo miradi ya nishati safi ya kupikia.
Chibulunje amesema, REA itahakikisha shule mbalimbali zinafungwa mfumo wa nishati safi wa kupikia na kuachana na matumizi ya kuni.
Amesisitiza kuwa wakala huo umesaini mikataba ya zaidi ya Sh. Bilioni 50 kuhakikisha taasisi zinazolisha watu zaidi ya 300 kama magereza na kambi za jeshi zinafungiwa mifumo ya nishati safi ya kupikia.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano kwa Umma kutoka REA, Martha Chassama amesema wakala umejipanga kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya matumizi sahihi ya nishati safi ya kupikia huku akiendelea kuhamasisha wananchi kuachana na matumizi ya nishati chafu ya kupikia.
“Rais amekuwa ni kinara katika kuhakikisha anaokoa Watanzania waliokuwa wanafariki au kupata madhara ya kiafya kutokana na matumizi ya nishati chafu ya kupikia. Na sisi REA tutaendelea kuhakikisha tunatoa elimu kwa umma ili lengo la kuhakikisha kufikia 2034 asilimia 80 au zaidi ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia,” amesema.
Awali mpishi wa shule hiyo, Said Ruanda
amesema wakati wanatumia kuni walikuwa wanatumia muda mwingi kuandaa chakula, juwepo wa joto na moshi.
“Kwa kweli kuna utofauti mkubwa sana toka tumeanza kupikia kwa kutumia gesi. Jikoni hamna moshi sana kama tulivyokuwa tunapikia kwa kuni lakini pia unaweza kupika ukiwa na nguo zako ulizokuja nazo na usichafuke tofauti na hapo zamani ilikuwa lazima ubadilishe nguo uvae nguo nyingine ili nguo zako ulizokuja nazo zisichafuke,” amesema.

You Might Also Like

Rais Samia akisikiliza jambo

Mtindi wa Korosho, Stafeli Wafanyiwa Utafiti UDSM

Kipanga: Lugha ya Kichina Inakuza Diplomasia, Kuimarisha Uhusiano

Jeshi la polisi kuchukua tahadhari mechi ya Simba, Yanga leo

Wasilisheni Migogoro Yenu Tume ya Usuluhishi na Uamuzi – Massawe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ridhiwani Kikwete Akagua Maandalizi ya Kilele Mbio za Mwenge Jijini Mwanza
Next Article SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?