MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari
Habari

Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: MWENDESHAJI Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari (WRF), Muchunguzi Kabonaki ameishauri jamii kujiunga na mfuko huo iweze kunufaika nao.
Mfuko huo upo Chini ya Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA).
Kabonaki ametoa ushauri huo alipozungumza na Gazeti la MFANYAKAZI akielezea jinsi mwanachama atakavyonufaika.
Amesema WRF unatoa mafao ya aina tano mojawapo likiwa ni fao  la kustaafu.
“Mwanachama aliyefikisha umri wa kisheria wa kustaafu kuanzia miaka 55 anapewa mafao, jumla ya michango yake na faida kwa kipindi alichokuwa mwanachama,” amesema.
Fao lingine linalotolewa na mfuko huo ni la kujitoa. Katika hilo Kabonaki amesema mwanachama aliyeamua kujitoa atapewa michango yake yote pamoja na faida zilizopatikana.
“Mwanachama anapojisajili kwenye mfuko hadi afikishe miaka miwili ndio ataruhusiwa kujitoa.
“Faida zinazopatikana za kiuwekezaji kila robo mwaka zitapelekwa kwenye akaunti yake,” amesema.
Kabonaki ameelezea fao lingine ni la kukosa kazi, kwamba mwanachama aliyepoteza kazi atapewa michango yake pamoja na faida.
Amesema mwanzo atapewa asilimia 50 kwa miezi mitatu ya kwanza, akiendelea kukosa kazi kwa miezi sita atapewa sehemu iliyobaki.
“Mfuko pia unatoa huduma ya “annuity”. Huu ni utaratibu ambao mwanachama ataweka fedha zake kwa mkupuo na kuingia makubaliano ya kulipwa kidogo kidogo kwa kipindi maalum. Katika kipindi hicho fedha ya mwanachama itaendelea kuzalisha faida kutoka kwenye uwekezaji ambao mfuko unafanya,” amesema.
Vile vile amesema kuna fao la wategemezi. Akifafanua hilo amesema wategemezi wa mwanachama aliyefariki watalipwa kulingana na kiwango kilichopo kwenye akaunti ya mwanachama pamoja na faida zote.
“Pia kuna manufaa ya kutumia michango ya mwanachama kama dhamana kwa ajili ya mikopo benki,” amesema.
Mfuko huo umeanzishwa mwaka jana kwa lengo la kutoa hifadhi ya jamii ya nyongeza kwa wanachama wa sekta rasmi na isiyo rasmi.

You Might Also Like

Mara Yapaa: Miaka Minne Ya Mafanikio Chini Ya Rais Samia

Majaliwa Asisitiza Matumizi ya Mifumo ya Kieletroniki Katika Makusanyo

Majaliwa Asisitiza Serikali Itaendelea Kuboresha Mazingira Ya Uwekezaji

Tanzania, Ufini Kushirikiana Teknolojia Za Kisasa Sekta ya Misitu

TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato
Next Article WDC Kuboresha Miradi Yake Ya Majengo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?