MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: SPIKA asisitiza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > SPIKA asisitiza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 
Habari

SPIKA asisitiza matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
SPIKA  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk Tulia Ackson amewataka wananchi  kutumia Nishati Safi ya Kupikia na kuachana na Nishati isiyo kuwa salama ili  kulinda afya zao, kutunza mazingira pamoja na kuondokana na athari za kijamii na kiuchumi .
Kauli hiyo imetolewa  wakati wa hitimisho la tamasha la mashindano ya mapishi ya vyakula kwa kutumia Nishati safi ya kupikia ( Tulia Cooking Festival) iliyofanyika jijini Mbeya.
“Lengo la kuandaa Tamasha hili ni kuongeza uhamasishaji kwa jamii kuhusu elimu na matumizi ya  Nishati Safi ya Kupikia na wote tunafahamu kwamba ajenda hii imebebwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan  ambaye ni kinara wa Nishati Safi ya Kupikia Afrika na sasa ametambuliwa pia duniani kwa ujumla.” Amesema Dkt. Tulia
Ameeleza kuwa tamasha hilo limehusisha Mamalishe na Babalishe 1,000 ambapo amewapongeza kwa kutumia Jukwaa hilo ili kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na kuzitaka taasisi mbalimbali nchini kuandaa matamasha kama hayo ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi.
Aidha, amewapongeza wadau  kwa  kudhamini Tamasha la Tulia Cooking Festival  ambao wamewezesha elimu ya Nishati Safi ya Kupikia kufikia wananchi wengi zaidi.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati,  Judith Kapinga amesema Serikali imeandaa Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia ili kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati hiyo ifakapo mwaka 2034.
“Serikali inaendelea na jitihada mbalimbali za kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa kutoa mitungi ya gesi ambapo  mwaka 2023 Serikali ilitoa zaidi ya mitungi 104,000 na mwaka huu inategemea kutoa mitungi 450,000.” Amesema Kapinga.
Ameongeza kuwa,  nishati safi za kupikia zipo za aina nyingi ikiwemo gesi, umeme, majiko banifu na majiko mengine, pia amesisitiza kuwa nishati safi ni bora kwa kuandaa chakula kuliko nishati nyingine kama kuni na mkaa.
Kuhusu kupunguza bei ya gesi, amesema Serikali inaendelea na mikakati ya kuwasaidia watu wengi waweze kutumia nishati hiyo kwa gharama nafuu na amezitaka kampuni za gesi kuendelea kufanya ubunifu ili kuhakikisha wananchi wananunua gesi kwa kiasi cha fedha walichonacho.

You Might Also Like

WCF Yaleta Utulivu Mahala Pa Kazi – Katambi

Rais Samia Afungua Barabara Ya Mbinga-Mbamba Bay Yenye Km 66-Ruvuma

CCCC Yaandaa Tamasha La Dragon Boat

Kamati Ya Bunge Yakagua Mradi Wa Nyumba NSSF

Mashimba: Tumieni Siku Zilizobaki Kujiandikisha

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dhibitini Magonjwa ya Mlipuko-Mchengerwa
Next Article Dkt. Biteko ashiriki kilele cha miaka 60 JWTZ
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?