MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TASU yaiomba serikali inunue meli kutoa ajira kwa mabaharia
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TASU yaiomba serikali inunue meli kutoa ajira kwa mabaharia
Habari

TASU yaiomba serikali inunue meli kutoa ajira kwa mabaharia

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi
CHAMA cha Mabaharia Tanzania (TASU), kinaiomba serikali inunue au kutengeneza meli hata moja kwa ajili ya mizigo nje ya nchi na kuileta Tanzania ili vijana wanaomaliza vyuo wapate ajira.
Kaimu Katibu Mkuu wa TASU, Hamis Urembo amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa Mfanyakazi.
Urembo ameomba ombi hilo kwa kuwa hivi sasa ajira za mabaharia zimekuwa chache, ilhal chuo cha bahari kikiwa kinazalisha wanafunzi wengi kila mwaka ambao wanazagaa mitaani kwa kuwa hakuna meli za kuwasaidia.
“Sasa hivi tuna kiwanda kinatengeneza meli. Itengenezwe meli au inunuliwe nje ya nchi.
“Hapo zamani tulikuwa na kampuni ya ushirikiano ya meli ya China na Tanzania. Tulikuwa na meli nyingi kama MV Ruaha, MV Urafiki,
“Kupitia chama cha mabaharia kila baada y miezi sita tulikuwa tunachukua mabaharia kwetu sisi, wanakwenda China, wanafanya kazi miezi sita, baada ya miezi sita wanapokezana, sisi tunafanya kazi kwa mkataba,” amesema.
Amesema bahati mbaya zile meli zimeuzwa, na hiyo kampuni ya China imeuza meli zote, japo bado ipo.
Amesema kama serikali ingeweza kukaa nao na kuanza upya ushirikiano uliokuwepo ili wanunue meli.
Kwa upande mwingine amesema, changamoto nyingine iliyopo katika fani hiyo hakuna mwongozo wa ajira kwa kutoa mfano kwamba  Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), inaweza kutangaza nafasi za kazi.
Kwamba wanahitaji mabaharia na wanatambua vyeti , inapofikia kwenye maslahi na malipo hawatambuliwi vyeti.
” Kwa mfano mtu anasoma chuo cha baharia anapata vyeti vyake na kuwa nahodha lakini akipata kazi haitwi nahodha anaitwa dereva wa vivuko.
“Hiyo ni changamoto ambayo inatufanya sisi tuwe na matatizo hayo,” amesema.
Pia amesema ni muhimu kuwe na sera ya bahari kuondoa changamoto mbalimbali.

 

 

You Might Also Like

Dkt. Mpango: Tumuige Nyerere kwa Kulinda Amani, Uhuru na Maadili ya Taifa

Tril.1.5/- Za Umeme Vitongojini: Ndejembi Awasihi Ma-RC Na DC Kusimamia Kwa Ufanisi Mradi

VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani

Jeshi La Zimamoto Yaimarisha Elimu Kwa Wananchi Kuhusu Matumizi Salama Ya Nishati Ya Kupikia

Jeshi La Polisi Kufanya Ukaguzi Wa Hali Ya Juu Kwa Mashabiki Katika Mechi Za Simba Na Yanga

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TASU yaiomba serikali inunue meli kutoa ajira kwa mabaharia
Next Article Tanzania,  na Taasisi ya BVGH kuimarisha huduma za saratani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mradi Wa Umeme Mpomvu-GGM Kuimarisha Upatikanaji Wa Umeme Na Kuchochea Shughuli Za Kiuchumi Geita- Salome
Habari September 4, 2026
Wahitimu 794 Wa Vyuo Vya Elimu Ya Juu Waomba Kujiunga VETA
Habari September 4, 2026
Taka za saluni zageuka dhahabu ya kijani: COSTECH yamulika safari ya David kutoka wazo hadi hataza
Makala September 4, 2026
Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wakazi Wa Kisiwa Cha Jibondo Mafia
Habari September 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?