Na Lucy Lyatuu,Morogoro
BARAZA la Michezo La Taifa (BMT) limesema linatumia Tamasha la nne la Kitaifa La Utamaduni 2026 linaloendelea mkoani Morogoro kutoa elimu kwa wananchi kuhusu michezo na namna wanavyoweza kunufaika na fursa za mashindano ya mpira wa miguu kwa Mataifa ya Afrika (AfCON) yanayotarajiwa kufanyika nchini mwakani 2027.
Ofisa Michezo Mwandamizi wa BMT, Charles Maguzu amesema hayo wakati akizungumza katika banda la BMT katika Tamasha la Utamaduni linaloendelea mkoani humo na kuongeza kuwa mashindano ya Afcon nin muhimu kila mtu anufaike na fursa zilizomo.

Amesema ni muhimu kila mwananchi kushiriki kdri awezavyo ili kunufaika kiuchumi kulingangana na shughuli itakayokuwa ikiendelea katika viwanja vilivyoko Arusha, Zanzibar na Dar es Salaam.
“Wananchi wote tunawapa elimu wajue fursa hio ni ya wote,kama kuna mtu ana biashara ya nguo ajipange aje avune fedha,wa Kuuza karanga ajipange na hata wenye hotel pia wa wajitokeze waone ni namna gani wanaweza kuhamasisha wageni watakaokuja wapate huduma,”amesema Maguzu.
Amesema pia wananchi wanapewa mbinu namna wanavyoweza kupata mitaji kwa ajili ya kufikia ndoto zao za kufanya biashara wakati wa mashindano hayo ambapo BMT inawaunganisha na taasisi za fedha kuchukua mikopo au kwenye Halmashauri kupata mikopo ile ya vijana na kunufaika.




Amesisitiza kuwa mashindano ya Afcon yanahamasisha watu kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini na kwamba ni muhimu kushangilia lakini kuhamasisha wageni kutembelea vivutio hivyo.
Kadhalika amesema wanatumia tamasha hilo kuhamasisha wananchi kutoacha kucheza michezo ya asili ambayo mababu wa zamani waliicheza jambo litakalosaidia kulinda utamaduni wa kila mmoja.


