MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TAMCU Yapaa Kwa Uwekezaji,Yafikisha Thamani Ya Sh  Bilioni Tano
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TAMCU Yapaa Kwa Uwekezaji,Yafikisha Thamani Ya Sh  Bilioni Tano
Habari

TAMCU Yapaa Kwa Uwekezaji,Yafikisha Thamani Ya Sh  Bilioni Tano

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu Dodoma
CHAMA Kikuu cha Ushirika Cha Tunduru (TAMCU) kimesema  kinajivunia thamani ya chama hicho kuongezeka kutoka Sh bilioni 1.5 hadi zaidi ya Sh bilioni tano kutokana na utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na kuimarika kwa shughuli za uzalishaji na biashara za ushirika.
Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na  ujenzi wa kiwanda cha  korosho katika wilaya ya Tunduru,jengo la utawala lenye ghorofa tano linaloghagimu sh bilioni saba.
Mjumbe wa Bodi wa chama hicho, Nurdin Chakilo  amesema hayo wakati akizungumza na waandishi   wa habari katika maonesho ya nanenane jijini Dodoma
Amesema mafanikio hayo ni sehemu ya mabadiliko makubwa yaliyofanywa na chama hicho, ikiwemo uendeshaji wa mfumo wa stakabadhi za ghala, uuzaji wa pembejeo za ruzuku na ujenzi wa miundombinu ya kuongeza thamani ya mazao.
Amesema mfumo  wa stakabadhi  umesaidia kurahisisha huduma kwa wakulima, hususan katika upatikanaji wa pembejeo, hatua ambayo imechangia kuongeza tija na uzalishaji wa mazao.
Habari Picha 13041
Amesema Chama kilikuwa kimetoka kuwa na thamani ya  sh bilioni 1.5, lakini sasa, kutokana na miradi inayotekelezwa na chama ya zaidi ya bilioni tano,” amesema.
Amesema chama hicho pia kinaendesha ghala na shughuli za pembejeo, huku kikiendelea na mipango ya kuwekeza katika miradi mikubwa inayolenga kuongeza thamani ya mazao na mapato ya wanachama.
Ameongeza kuwa chama hicho kina matarajio ya kuongeza zaidi uzalishaji katika msimu unaoendelea, huku kikihimiza wakulima kutumia vizuri fursa za pembejeo na huduma zinazotolewa kupitia ushirika.
Kuhusu ujenzi wa jengo amesema  linatarajiwa kuwa na ukumbi mkubwa wenye uwezo wa kuchukua zaidi ya watu 700, pamoja na maeneo mengine yatakayopangishwa kwa ajili ya kuongeza mapato ya chama.
Amesema hatua za awali za mradi huo tayari zimeanza, zikiwemo taratibu za upatikanaji wa vibali, ramani na maandalizi mengine muhimu kabla ya kuanza ujenzi.
Amewataka vijana nchini kutumia fursa zilizopo katika vyama vya ushirika na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo na uchumi wa nchi.
Amesema ushirika siyo mfumo unaohusu wazee pekee, bali ni sehemu ya uchumi inayohitaji ushiriki wa makundi yote, hususan vijana ambao wana nafasi kubwa ya kuleta mawazo na ubunifu mpya.
Ametoa wito kwa wananchi na wadau wanaotembelea Maonesho ya Nane Nane kufika katika banda la chama hicho ili kujifunza kuhusu huduma, miradi na fursa mbalimbali zinazotolewa na ushirika.

You Might Also Like

Majaliwa Amwakilisha Rais Samia Kwenye Kilele Cha Siku Ya Utumishi Wa Umma

Kamati Ya Bunge Ustawi Na Maendeleo Ya Jamii Yaridhishwa Wananchi Wanavyofikiwa

REA Yapamba Moto Uhamasishaji Matumizi Ya Umeme

Mbunge Ngorongoro Aiomba Serikali Kufungua Uchumi Loliondo

Soko La Kisasa La Nyamachoma Lazinduliwa Vingunguti

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Bidhaa Zinazozalishwa Nchini Zifikie Viwango Vinavyotakiwa Kukidhi Masoko-Balozi Mussa
Next Article
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TTCL Yatumia Nanenane Kuelimisha Kuhusu Huduma Ya Kuhifadhi Taarifa Kidijitali
Habari August 3, 2026
Nishati Ni Chachu Ya Kilimo, Uchumi Na Maendeleo  Ya Vijijini – Saidy
Habari August 3, 2026
August 3, 2026
Habari August 3, 2026
Bidhaa Zinazozalishwa Nchini Zifikie Viwango Vinavyotakiwa Kukidhi Masoko-Balozi Mussa
Habari August 2, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?