MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TVLA Yazalisha Chanjo ya Kudhibiti Homa ya Kutupa Mimba kwa Mifugo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TVLA Yazalisha Chanjo ya Kudhibiti Homa ya Kutupa Mimba kwa Mifugo
Habari

TVLA Yazalisha Chanjo ya Kudhibiti Homa ya Kutupa Mimba kwa Mifugo

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: WAKALA wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) umewataka wafugaji nchini kuchanja mifugo dhidi ya ugonjwa wa homa ya kutupa mimba, ukielezwa kuwa ni tishio kubwa kwa uzalishaji wa mifugo, uchumi wa wafugaji na afya ya binadamu.
Daktari Mtafiti wa Magonjwa ya Mifugo kutoka TVLA, Issack Mengele, amesema ugonjwa huo umeenea katika mifumo mbalimbali ya ufugaji, lakini umeonekana kwa kiwango kikubwa zaidi kwa ng’ombe wanaofugwa kwa mfumo wa malisho huria unaotumiwa na jamii nyingi za wafugaji na wakulima.
Amesema tafiti zinaonyesha maambukizi ni madogo kwa ng’ombe wanaofugwa ndani, lakini yanaongezeka kwa kiasi kikubwa katika mifumo ya ufugaji wa asili kutokana na mwingiliano wa mifugo na ukosefu wa hatua za kinga.
Mengele amesema hatari ya ugonjwa huo inaongezeka zaidi kwa binadamu, hususan katika jamii zinazotumia maziwa mabichi bila kuyachemsha, jambo linalochangia maambukizi ya ugonjwa huo kutoka kwa wanyama kwenda kwa watu.
Amefafanua kuwa wagonjwa wengi hupata homa ya muda mrefu ambayo mara nyingi huchanganywa na malaria au homa ya matumbo, hivyo kushindwa kupata matibabu sahihi kwa wakati.
“Ugonjwa huu unaweza kusababisha mtu kupoteza nguvu za kufanya kazi na wakati mwingine kupoteza maisha endapo hautatambuliwa mapema,” amesema.
Kwa upande wa mifugo, amesema ugonjwa huo husababisha ng’ombe kuharibikiwa na mimba, kupungua kwa uzalishaji wa maziwa na kuathiri uzazi, hali inayosababisha hasara kubwa kwa wafugaji na kudhoofisha ukuaji wa mifugo.
Amesema katika baadhi ya maeneo nchini kiwango cha maambukizi kinafikia kati ya asilimia 15 hadi 20, huku maeneo machache yakiripoti viwango vya hadi asilimia 30 au 40, ingawa bado hakuna takwimu za kitaifa kutokana na tafiti kufanyika katika nyakati na maeneo tofauti.
Mengele amesema Serikali kupitia TVLA imeanza kuzalisha chanjo ya Brucellosis kwa ajili ya ng’ombe, akieleza kuwa chanjo hiyo inapendekezwa kutolewa kwa ndama wa kike kabla hawajaanza kuzaliana ili kuwakinga dhidi ya maambukizi.
Amewataka wafugaji kutumia chanjo hiyo kama njia bora ya kuzuia ugonjwa badala ya kusubiri madhara yake, akisisitiza kuwa kinga ni nafuu kuliko hasara inayotokana na kupungua kwa uzalishaji na vifo vya mifugo.

You Might Also Like

Makampuni 408 Ya Tanzania Yaruhusiwa Kusafirisha Mazao Ya Kilimo Kwenda China

Halmashauri Ya Jiji La Dodoma Lawataka Wakulima Kutumia Nanenane Kujifunza Kilimo Cha Kisasa

TUCTA Yafuatilia Hotuba Ya Waziri Mkuu Bungeni

Mpango wa Shule Salama Unaongeza ulinzi Kwa Watoto

Rais Samia azindua bwawa la umwagiliaji Mtibwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Halmashauri Ya Jiji La Dodoma Lawataka Wakulima Kutumia Nanenane Kujifunza Kilimo Cha Kisasa
Next Article SmartDarasa: Tunda la Miaka 40 ya COSTECH Linalobadili Elimu ya Sayansi Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

SmartDarasa: Tunda la Miaka 40 ya COSTECH Linalobadili Elimu ya Sayansi Tanzania
Makala August 1, 2026
Dkt. Nchemba: TPHPA Yazidi Kuwafikia Wakulima
Habari August 1, 2026
BRELA Kutumia Maonesho Ya Nanenane Kutoa Huduma Kuhusu Mfumo Ulioboreshwa
Habari August 1, 2026
 Wanasheria Wa TANESCO Watakiwa Kuendelea Kusimamia Maadili Na Taaluma-Twange
Habari July 31, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?