Na Lucy Lyatuu,Dodoma
SERIKALI imesema katika kuboresha huduma za hali ya hewa Tanzania (TMA) zinazotolewa kwa sekta ndogo ya usafiri wa anga, TMA imekamilisha ufungaji wa mitambo miwili ya uangazi wa hali ya hewa katika viwanja vya ndege vya Mpanda na Pemba.
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawe amesema hayo wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa Bunge huku akiomba kuidhinishiwa jumla ya Sh trilioni 2.87 Kati ya fedha hizo, Sh 126,041,236,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Sh 2,746,696,846,000 ni fedha za Miradi ya Maendeleo.
Amesema , TMA imeendelea na ujenzi wa miundombinu ya hali ya hewa ikiwemo maabara ya uhakiki wa vifaa vya hali ya hewa (Calibration Center) Dar es Salaam ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 46
Amesema Kuendelea kuboresha huduma za hali ya hewa;Serikali kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imeendelea na utoaji na udhibiti wa huduma za hali ya hewa nchini.
Amesema katika Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27, Wizara imezingatia Dira 2050, llani ya Uchaguzi Mkuu ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2025, Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV 2026/27- 2030/31), Mpango wa Taifa wa Maendeleo kwa mwaka 2026/27, Mpango Mkakati wa Wizara wa Miaka Mitano (2026/27 – 2030/31 ) pamoja na maelekezo ya Viongozi Wakuu wa Serikali.

