Na Lucy Lyatuu,Dodoma
SERIKALI imesema Usafirishaji kupitia reli ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma umezidi kuimarika ambapo katika kipindi cha Julai, 2025 hadi Machi, 2026 jumla ya abiria milioni 2.51 walisafirishwa ikilinganishwa na abiria millioni 2.05 waliosafirishwa katika kipindi kama hicho kwa mwaka wa fedha 2024/25 sawa na ongezeko la asilimia 22.40.
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawe amesema hayo wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa Bunge huku akiomba kuidhinishiwa jumla ya Sh trilioni 2.87 Kati ya fedha hizo, Sh 126,041,236,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Sh 2,746,696,846,000 ni fedha za Miradi ya Maendeleo.
Amesema katika kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi 2026, TRC ilisafirisha jumla ya tani 102,452 za mizigo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Serikali ya kuanza usafirishaji wa mizigo kupitia reli ya SGR.
Amesema Katika hatua za kuunganisha miundombinu ya reli ya SGR na MGR, Serikali imeendelea na uunganishaji wa reli hizo katika eneo la Ruvu ili kuwezesha usafirishaji wa mizigo kutoka Bandari za Dar es Salaam na Tanga, ambap0 utekelezaji wake umefika asilimia 85.

Aidha, amesema ujenzi wa kuunganisha reli za MGR na SGR unaendelea katika eneo la Bahi kwa lengo la kuwezesha uhamishaji wa mizigo (transhipment) kati ya reli hizo 2 na unaendelea vizuri.
Profesa Mbarawa amesema Serikali inaendelea kuboresha Reli ya MGR kwa kubadilisha reli nyepesi na kuweka nzito, pamoja na kuongeza uwezo wa madaraja. Ukarabati huo unaendelea kupitia Mfuko wa Reli, ambapo hadi Machi 2026, kipande cha Kaliua-Mpanda kilikuwa kimekamilika kwa asilimia 32.72.
Amesema katika Kukabiliana na mafuriko yanayoathiri Reli ya MGR katika eneo la Kilosa-Kidete-gandu, Serikali imekamilisha ujenzi wa njia ya reli yenye urefu wa km 6.2 na daraja katika eneo la Godegode-Gulwe ambapo ujenzi umefikia asilimia 99.
Amesema Serikali kupitia TRC imeendelea na ujenzi wa Reli ya SGR ambapo hadi kufikia Machi, 2026 ujenzi wa kipande cha kwanza Dar es Salam Morogoro (km 300) na kipande cha pili Morogoro Makutupora (km 422) umekamilika kwa sehemu kubwa. Aidha, TRC inaendelea na utoaji wa huduma ya usafiri wa treni kwa vipande husika.
Amesema Kwa kipande cha Mwanza lsaka (km 341), ujenzi unaendelea na umefikia asilimia 68.77.
Amesema 39. hadi kufikia mwezi Machi 2026, ujenzi wa reli ya SGR katika kipande cha tatu: Makutupora – Tabora (km 368) na kipande cha nne: Tabora Isaka (km 165) unaendelea ambapo kazi mbalimbali zinazoendelea kutekelezwa.
Kwa ujumla ujenzi wa vipande hivi 2 umekuwa na changamoto kwa muda mrefu, ambazo zilisababisha utekelezaji wake kuwa na kasi ndogo. Hata hivyo, Serikali tayari imepata suluhisho la kukamilisha ujenzi wake kwa kupata mkop0 wenye masharti nafuu wa thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.277, sawa na takriban Shilingi trilioni 3.32.
Kadhalika amesema kuanzia Januari, 2026 TRC imefanikiwa kuanza kujitegemea kwa upande wa Mishahara na Matumizi Mengineyo (0C) bila uwezeshaji kutoka MfukO Mkuu wa Serikali. Kwa kipindi cha takriban miaka 10, kiasi cha Shilingi bilioni 12.92 kila mwaka kilikUwa kinatolewa na Serikali kwa TRC kwa ajili ya mishahara.

