MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kesi 100 Za Wananchi Zasikilizwa Na Kupatiwa Suluhu Katiba Na Sheria
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kesi 100 Za Wananchi Zasikilizwa Na Kupatiwa Suluhu Katiba Na Sheria
Habari

Kesi 100 Za Wananchi Zasikilizwa Na Kupatiwa Suluhu Katiba Na Sheria

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu,Dodoma
WIZARA ya Katiba Na Sheria imetatua kesi 100  ambazo ni changamoto  kutoka kwa wananchi katika maeneo mbalimbali  nchini ikiwemo  zinazohusu ardhi, mirathi, utapeli na ubabe.
Waziri wa Katiba Na Sheria, Juma Homera amesema hayo wakati akisikiliza kero za wananchi chini ya kipindi cha  nne cha Sema na Waziri na kwamba  utaratibu  wa kusikiliza wananchi utaendelea kufanyika mara tatu kwa mwezi.
Akizungumza, Homera amesema  wananchi wengi wamekuwa wakionewa  na kuwataka kuendelea kupiga simu kueleza malalamiko yanayowasibu ili waweze kupata unafuu wa maisha na kupata haki zao.
” Wananchi hawana ulazima wa kwenda mahakamani…kipindi cha Sema na Waziri ni fursa kwao kujinga na kuzungumza moja kwa moja na kiongozi wao ili kusaidiwa,” alisema Waziri Homera na kuongera kuwa simu zaidi ya 30 zimepokelewa katika kipindi hicho.
Amesema kipindi hicho kimekuwa kikisaidia wananchi na hio ni kutokana na wananchi wengi kushindwa kujua sehemunya kuzifikisha changamoto zinazowakabili hivyo wajue  wanaweza kunufaika na Wizara yao na kuondoa ukiritimba kwa wanaoonea wengine.
Ametaja miongoni mwa kesi zilizosikilizwa na kufanyiwa kazi kuwa ni pamoja na ile ya mwanamke aliyekuwa akifanyiwa vitendo vya ukatili kwa kupigwa na mume wake ambapo wizara imefuatilia na kumchukulia sheria mwanaume huyo na kuchukuliwa hatua.
Homera ametaja kesi nyingine kuwa ni  inayohusu mzabuni aliyejenga shule katika  halmashauri ya Nzega Tabora ambapo alikuwa akiidai Halmashauri hiyo fedha kwa muda mrefu bila mafanikio ambapo Waziri  ameweza kuzungumza na Mkurugenzi moja kwa moja  na kuahidi kufuatilia suala hilo na kumlipa mlalamikaji.
Shauri lingine ni  la mwanafunzi wa Taaisi yanTeknolojia tawila Mwanza ( DIT ),Mwanza ambapo alidahiliwa katika kozi ya   uhandisi lakini akapelekwa kozi nyingine ya  kilimo lakini baada ya Waziri kusikiliza shauri  hilo amehakikisha amerudishwa katika emfumo husika.
Homera amesema lipo shauri la mmiliki wa kiwanja  namba 35 block A eneo la Mchechere Mwanza ambapo mmiliki  amenyanga’anywa umiliki na hati yake kupewa mtu mwingine,ambapo ameahidi kupeleka timu yake ya wanasheria katika mkoa huo akishirikiana na  Mkuu wa mkoa huo ili kufikia muafaka.
Amesema mbali na shauri hilo wapo wananchi wengi wenye malalamiko kama hayo na hiyo ikionesha kuna uonevu mwinginunaofanyika kwa wananchi wengine wakitumia ubabe wa fedha kuumiza wengine na kwa kupitia kipindi hicho atahakikisha wananchi wanapatiwa haki zinazowastahili.

You Might Also Like

Rais TUCTA Apongeza Mfuko Wa NSSF Kwa Ongezeko La Thamani Hadi Trilioni 9

Manara: Sitapambana na Wafanyabiashara, Nitawatetea

Mwigulu: Wavivu, Wazembe, Wala Rushwa Serikalini Jiandaeni Na Fyekeo

VETA Yafanya Mageuzi Makubwa Yaliyowezesha Wengi Kuajiriwa

Rais Mwinyi Azindua Ripoti ya Jiolojia, Utafiti Madini zanzibar

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wizara Ya Elimu Yaomba Kuidhinishiwa Trilioni 2.3
Next Article Asilimia 26 Ya Wanawake Ndio Wanaoamini Kuwa Na Uhuru Wa Kufanya Maamuzi Ya Kufanya Shughuli Za Uchumi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Asilimia 26 Ya Wanawake Ndio Wanaoamini Kuwa Na Uhuru Wa Kufanya Maamuzi Ya Kufanya Shughuli Za Uchumi
Habari May 8, 2026
Wizara Ya Elimu Yaomba Kuidhinishiwa Trilioni 2.3
Habari May 7, 2026
Dkt. William Ruto Aipongeza NSSF Tanzania Kwa Uwekezaji wa Dola zaidi ya Milioni 51 Nairobi
Habari May 5, 2026
Ruto: Uwekezaji wa NSSF Nairobi ni mfano bora wa matumizi ya akiba
Habari May 5, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?