Na Lucy Lyatuu,Dodoma
WIZARA Ya Habari,Utamaduni Sanaa Na Michezo imewataka wanamitandao ya kijamii nchini kuhakikisha wanabeba taswira ya kulinda maadili ya mtanzania na kupambana na mmomonyoko unaolikabili Taifa.
Waziri wa Wizara hiyo, Paul Makonda amesema Hayo wakati akizindua Ofisi Ya Tawi la Dodoma kwa Jumuiya Ya Wanahabari Wa Mitandao Tanzania (JUMIKITA).
Akizungumza Makonda amewataka wanamitandao hao kutokukubali kutumia maudhui yasiyo na maadili katika kurasa zao za mitandao ya kijamii na hata kubeba wale ambao Wana nia ya kuharibu maadili ya Tanzania.
” Acha niseme ukweli Ili mbadilike… kuharibu maadili yetu sio jambo la kusifiwa lazima kila mmoja kutambua misingi ya Taifa na kuilinda Kwa nguvu kubwa,” amesema Makonda na kuongeza kuwa maudhui yanayochapishwa yazingatie Mila, desturi na misingi ya jamii ya kitanzania.
Amewataka Kila mmiliki wa mtandao wa kijamii kuwa na kamati ya nidhamu ya kuonyana kuhusu maudhui yanayowekwa kwenye kurasa zaohuku wakitambua kuwa habari zina nguvu sana.
” Muwe na mfumo wa kufuatiliana na kuwajibishana Ili Taifa lisonge mbele,” amesema Makonda na kuwataka wanamitandao kuweka mifumonya kuwajibishana wenyewe kwa wenyewe.
Aidha ametoa maelekezo Kwa wanamitandao kutoka Rais Dkt Samia Suluhu Hassan aliwataka wanamitandao kuandaa shindano ambalo litatemgeneza maudhui yatakayobadilisha nchi hususani kwenye ukuaji wa uchumi Nchini.
“Mwanamitamdao atakayeshinda katika shindano hilo,Rais Dkt Samia ameahidi kutoa zawadi ya mil 10,lengo kalamu ya wanahabari itumike kuwa wino wa dhahabu,” amesema Makonda.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa JUMIKITA, Shaban Matwebe amesema wanamitandao wako tayari kufanya kazi kwa bidii na kwamba ni wakati sasa kwa kundi hilo kutambuliwa na kuwa rasmi

