MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Hotuba ya Rais Samia Yachochea Miradi Mikubwa ya Viwanda na Bandari Bagamoyo – Mgalu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Hotuba ya Rais Samia Yachochea Miradi Mikubwa ya Viwanda na Bandari Bagamoyo – Mgalu
Habari

Hotuba ya Rais Samia Yachochea Miradi Mikubwa ya Viwanda na Bandari Bagamoyo – Mgalu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
Dodoma: MBUNGE wa Bagamoyo, Subira Mgalu, amesema Hotuba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imegusa kwa kina miradi ya kimkakati, hususan katika sekta ya viwanda na uwekezaji kwa manufaa ya Jimbo la Bagamoyo.
Mgalu ameyasema hayo wakati akichangia Hotuba ya Rais Samia katika uzinduzi wa Bunge la 13, kuelekea siku 100 za utekelezaji wa Awamu ya Sita, Kipindi cha Pili.
Habari Picha 11000
Amesema nia ya Rais Samia ni kuanzisha kongani nyingine ya viwanda katika Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo, mradi ambao ulianza kupimwa takribani miaka 15 iliyopita na wananchi wamesubiri kwa muda mrefu utekelezaji wake.
“Kwa mara ya kwanza, Desemba 30, 2025, Wilaya ya Bagamoyo ilimpokea Waziri wa Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, akiwa na wawekezaji sita, ambao walikabidhiwa hati ili ndani ya mwaka mmoja wajenge viwanda,” amesema.
Ameongeza kuwa ndani ya siku 100 za utekelezaji, tayari kuna ushahidi wa kuanza kwa ujenzi wa Bandari mpya ya Bagamoyo baada ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kusaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) wa ujenzi wa gati tatu.
Mgalu amesema miradi hiyo mikubwa imepelekwa katika Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo na kuomba wananchi waliopisha maeneo yao kwa ajili ya miradi hiyo walipwe fidia stahiki kwa wakati.
Ameeleza kuwa, licha ya kusubiri kwa muda mrefu, Serikali imeanza hatua za kusikiliza na kushirikisha wananchi wa maeneo ya Kondo, Mlingotini, Pande, Zinga, Tiseza na Kiromo.
“Kwa sasa, kutokana na dalili tulizoziona za miradi hii kuanza na maelekezo ya Serikali katika hatua za awali, tuna imani wananchi watalipwa fidia na kupewa makazi mbadala,” amesema.
Akizungumzia mustakabali wa Bagamoyo, Mgalu amesema kuwa kufuatia utekelezaji wa miradi mikubwa, ujenzi wa barabara ya Makofia–Mlandizi pamoja na kipande cha reli ya SGR kutoka Kwala hadi eneo la viwanda, ana imani kuwa ndani ya miaka mitano ijayo Bagamoyo itakuwa mji tofauti kabisa kimaendeleo.

You Might Also Like

UDOM yashauri matumizi ya green house kupata tija

Mkutano Maalum wa CCM Kufanyika Kesho Mtandaoni

TPHPA Tuna Mchango Mkubwa Katika Utoshelevu Wa Chakula – Ndunguru

Dira za Maji Kumaliza Kero ya Ankara

Uteuzi: Abubakar Mombo Ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Siwa amestaafu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge Ndoinyo Asema Imani ya Wananchi kwa Rais Samia Yazidi Kuimarika
Next Article PSPTB Yatangaza Matokeo ya Mitihani ya 32, ,Yawataka Waliokoa Alama Kujisajili Upya 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari February 2, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?