MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: MBUNGE wa Kasulu Mjini Ahoji Serikali Kuhusu Mradi wa Maji Mwanga B
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > MBUNGE wa Kasulu Mjini Ahoji Serikali Kuhusu Mradi wa Maji Mwanga B
Habari

MBUNGE wa Kasulu Mjini Ahoji Serikali Kuhusu Mradi wa Maji Mwanga B

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
1 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBUNGE wa Kasulu Mjini, Profesa Joyce Ndalichako, ameiuliza Serikali kuhusu mpango wake wa kuanza utekelezaji wa mradi wa usambazaji maji katika eneo la Mwanga B, jimboni humo.
Profesa Ndalichako alihoji swali hilo bungeni jijini Dodoma, akitaka kujua lini mradi huo utaanza rasmi.
 “Je, Serikali itaanza kutekeleza Mradi wa Usambazaji Maji Mwanga B katika Jimbo langu la Kasulu?” alihoji mbunge huyo.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Maji,  Mathew Kundo, alisema Serikali tayari imeanza utekelezaji wa mradi huo uliopo mjini Kasulu, mkoani Kigoma.
Kundo aliongeza kuwa mkandarasi wa mradi tayari amesambaza mabomba yote yenye urefu wa kilometa 52 katika eneo hilo.
Aidha, kazi nyingine zinazotarajiwa ni pamoja na kubadili mfumo wa nishati kutoka jua kwenda gridi ya umeme kwa ajili ya uzalishaji wa maji, pamoja na ujenzi wa chemba za ukaguzi wa mtandao wa mabomba.
“Mheshimiwa Spika, mradi huu utakapokamilika unatarajiwa kunufaisha wananchi 68,000 wa mitaa sita ya Mwanga B, Muganza, Msambara, Nyachidima, Kimwobwa na Kigondo,” alisema Kundo.
Aliongeza kuwa Serikali itahakikisha inapeleka fedha za kutosha kwa ajili ya mradi huo ili ukamilike na kuanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi waliokusudiwa kufaidika.

You Might Also Like

UDSM  Kujenga Jengo La Kisasa La Bil 8.3

NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani

Naibu Waziri Katambi Asisitiza Ufanisi na Ubunifu Kwenye SIDO

Fikeni kwa wakati CMA, mtatuliwe migogoro ya kikazi – Massawe

LATRA Kuwapiga ‘Stop’ Wasiokamilisha Utaratibu, Tiketi Mtandao

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dkt. Majule Ahoji Hatua za Kulinda Wananchi Dhidi ya Mikopo Hatari
Next Article Waziri Mkuu Asisitiza Elimu ya Bima ya Afya kwa Wote Vijijini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
Serikali Yaendelea Kuimarisha Uhuru wa Mahakama – Nchimbi
Habari February 2, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?