MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TADB Yatoa Elimu ya Kifedha kwa Wananchi na Wanafunzi Tanga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TADB Yatoa Elimu ya Kifedha kwa Wananchi na Wanafunzi Tanga
Habari

TADB Yatoa Elimu ya Kifedha kwa Wananchi na Wanafunzi Tanga

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetumia maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa kutoa elimu ya kifedha kwa wananchi na wanafunzi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga jamii yenye uelewa mzuri wa masuala ya fedha na maendeleo ya kiuchumi.
Akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho hayo yanayoendelea mkoani Tanga, katika viwanja vya Usagara, Ofisa Maendeleo wa Biashara wa TADB Kanda ya Kaskazini, Irene Kasegezya, alisema benki hiyo imekuwa ikitoa elimu ya kifedha kwa makundi mbalimbali tangu kuanza kwa maonyesho hayo Januari 19, 2026.
Kasegezya alisema hadi sasa TADB imewahudumia wananchi wengi, wakiwemo wanafunzi zaidi ya 200, waliopatiwa elimu ya kifedha itakayowasaidia kujenga msingi imara wa usimamizi wa fedha kwa maisha yao ya sasa na ya baadaye.
Alisema elimu hiyo inalenga kuwajengea wanafunzi nidhamu ya kifedha mapema na kuwaandaa kuwa na desturi chanya za kifedha.
Aliongeza kuwa wananchi waliotembelea banda la TADB wamepata fursa ya kushiriki mafunzo kuhusu upangaji wa matumizi, utunzaji wa kumbukumbu za fedha pamoja na maandalizi ya kupata mikopo.
Aidha, alibainisha kuwa elimu ya kifedha ni muhimu kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, kwani huwasaidia kupanga shughuli zao kiuchumi na kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa yanafanyika mkoani Tanga chini ya kaulimbiu isemayo ‘Elimu ya Kifedha ni Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii.’.
Kasegezya aliwahimiza wananchi kuendelea kutembelea banda la TADB ili kupata elimu, ushauri wa kitaalamu na taarifa kuhusu huduma za benki hiyo.

You Might Also Like

Lugha ya Kichina Ni Ufunguo wa Fursa za Kimataifa – Profesa Maisel

TFS Yawataka Wananchi Kufuga Nyuki Kuzuia Uharibifu Wa Mazingira

UDSM Yapiga Hatua Kubwa Kuboresha Miundombinu na Mitaala kwa Mradi wa HEET

Umeme Jua Kuchoche Uchumi Maeneo Ya Vijijini

Watafiti Mataifa 10 Kujadili ElimuMsingi Nchini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article SANGU: e-Utatuzi Italeta Mapinduzi katika utoaji Haki
Next Article DIB: Wenye Amana Benki Zilizofungwa Kulipwa Ndani ya Mwezi Mmoja
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Kisasa Design: Kampuni ya Kitanzania Inayobadilisha Sekta ya Interior Design na Utengenezaji wa Samani
Habari June 6, 2026
Vidukari Hatari Vyafuatiliwa Mikoa 17 Kulinda Zao la Mpunga
Makala June 5, 2026
KARIBU ESCAPE LODGE SERENGETI – NYUMBA YAKO YA KIFAHARI KATIKATI YA UFALME WA WANYAMAPORI
Habari June 5, 2026
Sheria Ya  Kuzuia Shisha Kutungwa, Yabainika Kuwekwa Dawa Za Kulevya
Habari May 29, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?