MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TRA Yatoa Zawadi Za Krismas Na Mwaka Mpya Kwa Watoto Wenye Mahitaji
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TRA Yatoa Zawadi Za Krismas Na Mwaka Mpya Kwa Watoto Wenye Mahitaji
Habari

TRA Yatoa Zawadi Za Krismas Na Mwaka Mpya Kwa Watoto Wenye Mahitaji

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu

KAMISHNA wa Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuf Mwenda anawasihi walipa kodi nchini kuendelea kulipa kwa hiari kwa kuwa michango yao husaidia jamii kupata mahitaji yao hususan makundi maalum.
Mwenda amesema hayo wakati akikabidhi shehena ya zawadi za Krismas na Mwaka Mpya kwa Kituo cha Udiakonia cha Kulea Watoto Wenye Ulemavu wa akili cha Mtoni, Temeke na kwa Makao ya Kulea Watoto Yatima Hisani yaliyopo Kibada Kigamboni, Dar es Salaam.
Habari Picha 10766
Zawadi zilizotolewa kwa makundi hayo ni pamoja na sukari, mafuta, sabuni, unga, chumvi, vifaa mbalimbali vya usafi, vifaa vya watoto, vyakula na hata fedha .
Akizungumza katika Kituo cha Udiakonia Mtoni, Mwenda amewapongeza  viongozi wa kituo hicho kinachosimamiwa na Kanisa La Kiinjili La Kiluther Tanzania (KKKT)  kwa malezi yanayotolewa kwa watoto hao kwani yana mchangokubwa
Habari Picha 10767

kwao.

Amesema  walipa kodi wamekuwa na mchango mkubwa kwa watanzania ambapo hutumika pia kusaidia makundi maalum kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.
Mwenda amewaomba kuendelea kulipa kodi  ambayo pia hutumika kuendeleza jamii kwa njia moja hadi myingine.
Kwa upande wake Mratibu wa Kituo hicho Winifrida Malumbo amesema kituo hicho kinasimamiwa na KKKT pamoja na serikali na lengo kubwa ni kuhakikisha hakuna kundi linaloachwa nyuma.
Amesema  kituo kina watoto 107 wakifundishwa program mbalimbali ili kuweza  kujitegemea wenyewe na mzazi huweza kujifunza stad mbalimbali za malezi.
Amesema pia watoto hao hufundishwa elimu maalum, wakipata huduma ya upimaji ili kubaini aina ya changamoto zinazowakabili pamoja na huduma ya matendo mema kwa wenye uhitaji.
Mchungaji wa Usharika wa Mtoni Salome Mwaisenge ameshukuru TRA kwa msaada huo katika kusherehekea sikukuu hizo.
Habari Picha 10768
Katika Makao Ya Watotoyajulikanayo kama Hisani, Mwenda amesema kazi ya malezi ni ya jamii yote na kuwashukuru walipa kodi na kwamba kutoa zawadi kama hizo mi ishara ya kutambua mchango wao.
“Kipindi hiki ni cha kushukuru walipa kodi wote Tanzania kwa kuwa mchango wao unatumika pia kusaidia jamii, ” Amesema na kusisitiza uongozi wa Makao kusimamia watoto kusoma kwa bidii.
Amesema yuko tayari kuwa balozi wa kuwasemea watoto wanaomaliza masomo wakitoka katika kituo hicho ili waweze kupata kazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Makao hayo Hidaya Mwakitalema amesema watoto wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kukosa usafiri kwa ajili ya kupeleka watoto hospitalini pindi ikitokea tatizo na hata kukosa bima ya afya kwa watoto hao.

You Might Also Like

TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa

Profesa Laizer Kupambana Na Umaskini, Ujinga, Maradhi

TEITI Yashiriki Maonesho ya Nane ya Uwekezaji Sekta ya Madini Geita

Wahifadhi Saohill Wapongezwa

Mgombea Urais Wa CCM, Dkt. Samia Aendelea Na Kampeni Temeke

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Lugha ya Kichina Ni Ufunguo wa Fursa za Kimataifa – Profesa Maisel
Next Article Waziri Sangu, Balozi UAE Wajadili Fursa za Ajira kwa Watanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?