MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Viongozi Watakiwa Kuweka Haki Mbele Katika Kusimamia Masuala ya Wafanyakazi — COWTU (T)
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Viongozi Watakiwa Kuweka Haki Mbele Katika Kusimamia Masuala ya Wafanyakazi — COWTU (T)
Habari

Viongozi Watakiwa Kuweka Haki Mbele Katika Kusimamia Masuala ya Wafanyakazi — COWTU (T)

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHAMA cha COWTU (T) kimesema kuwa viongozi wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi ya haki na uwajibikaji.

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Mussa Mwakalinga, ameyasema hayo leo Novemba 25, 2025, wakati akifunga mafunzo kwa watendaji wa chama hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa TUCTA, Makao Makuu.

“Kama viongozi, ni vizuri kutambua kuwa uongozi tuliopewa ni tunu na neema kutoka kwa Mungu. Hivyo, yatupasa kuzingatia majukumu yetu kwa kutenda haki,” amesema.

Habari Picha 10433

Mwakalinga ameeleza kuwa majukumu ya COWTU (T) ni kudai kulinda na kutetea haki, maslahi, heshima, hadhi na utu wa wanachama wake.

Amewataka viongozi kuhamasisha wafanyakazi kujiunga na chama hicho, kutoa elimu kwa wanachama, kutoa huduma mbalimbali na kushughulikia migogoro sehemu za kazi.

Aidha, amewataka viongozi kuhakikisha matawi ya chama yanakua na kusimamiwa kwa nidhamu, huku wakitumia ipasavyo wasimamizi wa kazi.

Naye Katibu wa chama hicho Kanda ya Mashariki, Seka Kitori, amesema vyama vya wafanyakazi vinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ushirikiano.

Habari Picha 10430

“Tunapotembea kwa pamoja, tuhakikishe tunatembea kwa pamoja kwa uhalisia. Ni vizuri idara ya kazi ikatekeleza wajibu wake,” amesema.

Kwa upande wake, Subira Mwasamboma kutoka Idara ya Rasilimali Watu amesema kuwa kuna haja ya mabadiliko katika masuala yanayohusu vyama vya wafanyakazi.

Habari Picha 10434

Naye Ofisa Elimu Msaidizi, Nancy Mwansasu,amesema kuwa baadhi ya changamoto zilizopo zinahitaji viongozi wenyewe kuanza kubadilika. “Tunahitaji mabadiliko,” amesema.

Mafunzo hayo yalijikita katika mada mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya sheria za kazi na utekelezaji wake, historia ya vyama vya wafanyakazi, kuanzishwa kwake, majukumu yake, uhusiano kati ya vyama, serikali na waajiri, pamoja na mbinu za utatuzi wa migogoro sehemu za kazi.

Habari Picha 10436
Habari Picha 10433
Habari Picha 10431
Habari Picha 10433

You Might Also Like

Wananchi Wahimizwa Kulinda Maeneo Yaliyohifadhiwa  Kisheria- Kamishna  Wakulyamba

Dar Sasa Kufanya Biashara Saa 24, Kuanza Februari 22 Mwaka Huu

Polisi Dodoma Yawataka Wananchi Kutoa Taarifa 

Dendego Achangisha Bilioni 1.7, Ujenzi Ofisi Ya CCM

Jaffo Aagiza Kufufuliwa Vilivyokuwa Viwanda Vya Serikali

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Huduma za Maktaba Zabadilika: Malipo Kidijitali, Usomaji Mtandaoni
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Huduma za Maktaba Zabadilika: Malipo Kidijitali, Usomaji Mtandaoni
Habari November 25, 2025
Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?