MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari

Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha Tanzania inazalisha nguvukazi yenye ujuzi, ubunifu na umahiri unaokidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye ya soko la ajira na maendeleo ya viwanda.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wamiliki wa viwanda, waajiri na wadau wa elimu ya ufundi stadi, Profesa Nombo amesema Sera ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya 2014 (Toleo la 2023) imeweka mkazo katika kujenga mfumo wa elimu unaozingatia ujuzi na tija kwenye soko la ajira.
Habari Picha 10047
Amesema kupitia sera hiyo, Serikali imeendelea kuimarisha ubora wa mafunzo, kuongeza ushirikiano kati ya taasisi za elimu na sekta binafsi, na kuhakikisha wananchi wanapata fursa sawa za kujifunza na kujiendeleza.
Kwa mujibu wa Profesa Nombo, VETA ina zaidi ya vyuo 900 vinavyotoa mafunzo kwa zaidi ya wanafunzi 300,000 kwa mwaka, huku Serikali ikiendelea kujenga vyuo vingine 64 ili ifikapo mwaka 2026 kuwe na vyuo 145 kote nchini.
Amesema ushirikiano wa VETA na sekta binafsi umewezesha wanafunzi kupata mafunzo ya vitendo kwenye viwanda, migodi na hoteli, ikiwa ni pamoja na makampuni kama Geita Gold Mining, Barrick na North Mara, jambo linalowawezesha vijana kujifunza kwa vitendo na kujiajiri.
Ameongeza kuwa hadi mwaka 2024 Tanzania ilikuwa na zaidi ya viwanda 8,400, ikiwemo zaidi ya 200 vikubwa, vinavyochangia ajira na pato la Taifa, na kwamba ajira zaidi ya 700,000 zinatarajiwa katika sekta za viwanda, ujenzi na nishati ndani ya miaka mitano ijayo.
Profesa Nombo amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya VETA, waajiri na viwanda ili kuhakikisha vijana wanapata ujuzi unaokidhi mahitaji ya uchumi wa viwanda.
Habari Picha 10046
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Anthony Kasore amesema serikali inawahitaji kuhakikisha elimu ya ufundi stadi inakuwa shirikishi, wanaosoma wakienda kwenye ajira waendane na mahitaji ya soko.
Amesema umuhimu wa wadau ni kuhakikisha VETA inatoa elimu bora, lakini ili kufikia huko wanaanzia kwenye mitaala hivyo ni lazima kukutana nao na kuona namna bora ya kuandaa mitaala hiyo.
“Naomba wadau mbalimbali wa elimu ya ufundi stadi kuendelea kuunga mkono juhudi za kuimarisha kupata mafunzo yanayoendana na soko,” amesema.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Clotilda Ndezi alimwakilisha Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Profesa Sifuni Mchome kwa kusema bodi hiyo inaendelea kutoa msukumo kuhakikisha mafunzo ya ufundi stadi nchini yanakuwa ya vitendo zaidi na yanayoendana na mahitaji ya soko la ajira.
Habari Picha 10050
“Bodi imesisitiza katika sera zake na miongozo kuwa mitihani na tathmini za wanafunzi zijikite zaidi kwenye vitendo kuliko nadharia,” amesema.

You Might Also Like

Jeshi La Uhifadhi Wasisitizwa Kuzingatia Misingi ya Haki za Binadamu

Tanzania Ipo Tayari Soko la Pamoja kuuziana Umeme – Biteko

Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija

Wahamasika Kutumia Mbegu Bora Za Karanga Zilizofanyiwa Utafiti Na TARI

FCC Yawavutia Wawekezaji Kwenye Maonesho Ya IATF Nchini Algeria

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Yapeleka Sh Bil 10 Kwa Kiwanda Cha Viuadudu Cha TBPL
Next Article Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Serikali Yapeleka Sh Bil 10 Kwa Kiwanda Cha Viuadudu Cha TBPL
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?