MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Habari

Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Umoja Wasisitizwa Kama Msingi Wa Mtangamano Wa SADC

Na Mwandishi Wetu

ANTANANARIVO, MADAGASCAR: UMOJA na mshikamano vimeelezwa kuwa silaha kuu ya kuimarisha mtangamano wa kweli ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kufuatia makabidhiano rasmi ya uenyekiti wa Kikao cha Maofisa Waandamizi kutoka Zimbabwe kwenda kwa Madagascar.

Makabidhiano hayo yalifanyika Agosti sita, mwaka huu 2025 jijini Antananarivo, ambapo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Madagascar, Eric Ratsimbazafy, amepokea uenyekiti kutoka kwa Balozi Albert Chimbindi wa Zimbabwe, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa.

Katika hotuba yake ya kuaga, Balozi Chimbindi ameeleza kuwa licha ya changamoto za kimataifa kama UVIKO-19, ukame, na mabadiliko ya tabianchi, SADC imeendelea kuwa imara kiuchumi na kunufaika katika nyanja za ulinzi, usalama, viwanda na huduma za kijamii.

Ametoa wito kwa nchi wanachama kushirikiana zaidi katika ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, nishati na maji ili kuongeza kasi ya maendeleo na ajira kwa vijana, akisema rasilimali watu na maliasili ni nguzo muhimu za ustawi wa kanda.

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Amina Khamis Shaaban.

Kikao hiki ni miongoni mwa vikao vya maandalizi kuelekea Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika Agosti 17, 2025.

You Might Also Like

Wananchi Wahimizwa Kulinda Maeneo Yaliyohifadhiwa  Kisheria- Kamishna  Wakulyamba

Biashara kidijitali inawezekana soko huru la Afrika

Rais Mwinyi Ajionea Mifumo Mbalimbali Banda La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba

Stamico Yapewa Tuzo Na FDH Kujali Wenye Ulemavu

VETA Shinyanga Yatumia Kompyuta Kubuni Bidhaa 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji
Next Article Mafua, Kifua Yadaiwa Kusababisha Kifo cha Job Ndugai
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchimbi Ahimiza Ushirikiano wa Wizara Katika Uhifadhi wa Mazingira
Habari March 10, 2026
Mtaka, Ndunguru Wakubaliana Ujenzi wa Maabara ya Kimkakati Njombe
Habari March 10, 2026
Wataalamu wa Fedha SADC Wakutana Pretoria Kujadili Bajeti
Habari March 9, 2026
TASFAM Yawawezesha Wanawake wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Kuadhimisha Siku ya Mwanamke
Habari March 9, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?