MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Habari

Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Umoja Wasisitizwa Kama Msingi Wa Mtangamano Wa SADC

Na Mwandishi Wetu

ANTANANARIVO, MADAGASCAR: UMOJA na mshikamano vimeelezwa kuwa silaha kuu ya kuimarisha mtangamano wa kweli ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kufuatia makabidhiano rasmi ya uenyekiti wa Kikao cha Maofisa Waandamizi kutoka Zimbabwe kwenda kwa Madagascar.

Makabidhiano hayo yalifanyika Agosti sita, mwaka huu 2025 jijini Antananarivo, ambapo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Madagascar, Eric Ratsimbazafy, amepokea uenyekiti kutoka kwa Balozi Albert Chimbindi wa Zimbabwe, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa.

Katika hotuba yake ya kuaga, Balozi Chimbindi ameeleza kuwa licha ya changamoto za kimataifa kama UVIKO-19, ukame, na mabadiliko ya tabianchi, SADC imeendelea kuwa imara kiuchumi na kunufaika katika nyanja za ulinzi, usalama, viwanda na huduma za kijamii.

Ametoa wito kwa nchi wanachama kushirikiana zaidi katika ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, nishati na maji ili kuongeza kasi ya maendeleo na ajira kwa vijana, akisema rasilimali watu na maliasili ni nguzo muhimu za ustawi wa kanda.

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Amina Khamis Shaaban.

Kikao hiki ni miongoni mwa vikao vya maandalizi kuelekea Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika Agosti 17, 2025.

You Might Also Like

Kadogosa: Serikali Yatenda Haki Kwa Wakulima, Wafugaji, Wananchi Wa Vijijini

TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge

BAKITA Lapongeza Sheria Za Tanzania Kuandikwa Kwa Lugha Ya Kiswahili

REA Yatoa Milioni 38.2 kwa ajili ya kufungwa mfumo wa nishati safi, Shule ya Samia

Waziri Ridhiwani: Vyama Vya Wafanyakazi, Nguzo Ya Mahusiano Mema Mahali Pa Kazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji
Next Article Mafua, Kifua Yadaiwa Kusababisha Kifo cha Job Ndugai
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?