MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Zabibu Ya Makutupora Nyekundu Yatajwa Kuwa Ya Kipekee Duniani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Zabibu Ya Makutupora Nyekundu Yatajwa Kuwa Ya Kipekee Duniani
Habari

Zabibu Ya Makutupora Nyekundu Yatajwa Kuwa Ya Kipekee Duniani

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
DODOMA: WATAFITI kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) wameitaja mbegu ya zabibu aina ya Makutupora Nyekundu kuwa ina sifa za kipekee zinazoiweka katika daraja la juu duniani.
Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja cha redio jijini Dodoma leo Julai 30, 2025 Mtafiti Mwandamizi kutoka TARI Kituo cha Makutupora,  Felista Mpore amesema mbegu hiyo imekuwa ya kipekee kutokana na kiwango kikubwa cha sukari kinachopatikana ndani yake.
“Mbegu ya Makutupora Nyekundu ina uwezo mkubwa wa kutoa sukari kwa kiwango cha juu, ambacho ni miongoni mwa viashiria muhimu vya ubora katika sekta ya usindikaji wa zabibu,” amesema.
Mbali na kiwango cha sukari, mbegu hiyo pia ina uwezo wa kustahimili magonjwa, kuhimili ukame, kutoa mavuno mengi, pamoja na kuwa na rangi mbalimbali zinazovutia watumiaji.
Kwa mujibu wa Mpore, watafiti kutoka mataifa mbalimbali wamekuwa wakifika nchini kuchukua sampuli za vinasaba kwa ajili ya kulinganisha na aina nyingine za zabibu duniani, ambapo matokeo yamebainisha kuwa Makutupora Nyekundu ina sifa za kipekee zinazoiweka katika kundi la zabibu bora zaidi duniani.
Katika kuunga mkono jitihada za kuongeza thamani ya zao hilo, TARI imeendelea kutoa mafunzo kwa wakulima na wadau wa sekta ya kilimo, ikilenga kuwajengea uwezo katika kuongeza tija kupitia usindikaji na masoko ya kisasa.
“Tunawahimiza wakulima wajikite katika kuongeza thamani ya zabibu badala ya kuuza ghafi. TARI itaendelea kutoa elimu na mafunzo, hususan kuelekea Maonesho ya Kilimo ya Nanenane ambapo tutakuwepo katika viwanja mbalimbali, ikiwemo vile vya kitaifa vilivyopo Nzuguni, Dodoma,” amesema.
Zabibu ya Makutupora Nyekundu hulimwa kwa wingi katika maeneo ya kati nchini Tanzania, hususan Mkoa wa Dodoma, na imekuwa chanzo kikuu cha malighafi kwa viwanda vya ndani vya utengenezaji wa mvinyo.

You Might Also Like

TTCL Kuboresha Mifumo Kwa Kutumia Teknolojia Za Kisasa

Vyama Vya Wafanyakazi Kujadili Hatma Ya Wafanyakazi TAZARA

OUT yaunda Kamati ya Ufuatiliaji na Tathmini Mradi wa HEET

Sheria Ya Kupata  Taarifa, Ya NGOs Zina Upungufu 

OUT Yasaini Mkataba Ujenzi Wa Maabara Tatu Za Sayansi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais CWT Ni Kiongozi Aliyekuza Taaluma Kwa Moyo, Sio Cheo
Next Article Wagombea Wa CCM Dodoma Mjini Waanza Kujinadi kwa Wajumbe
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?