MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Waziri Mbarawa Aagiza Adhabu Kali kwa Madereva, Makondakta Wanaonyanyasa Wanafunzi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Waziri Mbarawa Aagiza Adhabu Kali kwa Madereva, Makondakta Wanaonyanyasa Wanafunzi
Habari

Waziri Mbarawa Aagiza Adhabu Kali kwa Madereva, Makondakta Wanaonyanyasa Wanafunzi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Lucy Ngowi
DODOMA: WAZIRI wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) kutoa adhabu kali kwa madereva na makondakta watakaobainika kuwanyanyasa wanafunzi.
Profesa Mbarawa alitoa agizo hilo leo Februari 4, 2026, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuboresha usafiri wa wanafunzi katika miji.
Amesema LATRA inapaswa kuhakikisha madereva na makondakta wote wanathibitishwa na kusajiliwa, huku wakidhibiti nauli, staha ya huduma, na usalama wa wanafunzi kwa wakati wote.
Pia alisisitiza kutoa elimu kwa watoa huduma ili wafuate haki na wajibu wao.
Habari Picha 11072
Aidha, Wizara ya Uchukuzi imeagiza ziwepo namba za bure kwenye treni za abiria, daladala, na mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani ili abiria waweze kuripoti malalamiko kwa urahisi.
Profesa Mbarawa pia aliagiza kushirikiana na Jeshi la Polisi kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na wa kushtukiza katika vituo vya daladala, hasa nyakati za asubuhi na jioni.
Agizo hilo limekuja baada ya video iliyosambaa mitandaoni ikionyesha binti Mariana Mirindima, mwanafunzi wa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Jangwani, akiwasilisha barua inayoripoti changamoto wanazokutana nazo wanafunzi.
Katika barua yake, Mariana alieleza kuwa makondakta wanagoma kuwabeba wanafunzi wakidai kuwa hawalipi nauli kamili, hali inayowalazimisha kusubiri muda mrefu njiani, kuchelewa shuleni, na kukosa usalama.
Mwanafunzi huyo aliomba wizara ichukue hatua stahiki dhidi ya watoa huduma wa daladala ili kuhakikisha wanafunzi wanapata haki yao ya msingi ya elimu na usafiri salama.

You Might Also Like

TEA Kukarabati Jengo La Bodi Ya Maktaba Kwa Milioni 300

Someeni fani zisizo maarufu – mwalimu

Tanzania Yaongoza Kwa Ushiriki, Makongamano Ya Ushirika Ndani, Nje Ya Nchi

Manyara Kusambaza Mitungi 16,275 ya Gesi kwa Bei ya Ruzuku

Baraza Kuu TUGHE Lasisitiza Haki, Wajibu Kuleta Tija Sehemu Za Kazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Next Article Katoro Yapata Gari Jipya la Zimamoto, Kuwasili Februari 9
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Katoro Yapata Gari Jipya la Zimamoto, Kuwasili Februari 9
Habari February 4, 2026
Mbunge Asisitiza Sheria za Majiko Safi Ili Kulinda Mazingira
Habari February 3, 2026
Mwalunenge: Bila Rasilimali Watu Na Mtaji, Mipango Ya Kilimo Haitafanikiwa
Habari February 3, 2026
Gulamali Ahoji Bungeni Changamoto ya Mawasiliano Ilongelo
Makala February 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?