MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Watafiti, Wabunifu Waendelezwe Wasivunjwe Moyo- Biteko
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Watafiti, Wabunifu Waendelezwe Wasivunjwe Moyo- Biteko
Habari

Watafiti, Wabunifu Waendelezwe Wasivunjwe Moyo- Biteko

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: SERIKALI imeagiza kuwatumia wanasayansi wa ndani ya nchi badala ya kuwavunja moyo kwa kuwa wanafanya kazi nzuri ya kutatua changamoto zilizopo katika jamii.
Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri Mkuu. Dkt. Dotto Biteko leo Disemba mbili, 2024 alipomwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kufungua Kongamano la tisa la Sayansi, Teknolojia, Ubunifu na maonesho linaloendelea Jijini Dar es Salaam.
Amesema, “Umefika wakati kwa Serikali, taasisi na Mashirika kutambua, kuthamini na kutumia tafiti za wanasayansi wa ndani ya nchi ili kutatua changamoto zilizopo,”.
DKt. Biteko amesema wanasayansi nchini wanafanya kazi nzuri na kubwa ya kutafuta suluhu ya matatizo mbalimbali katika jamii lakini kazi zao zinatambuliwa zaidi nje ya nchi kuliko zinavyotambuliwa nchini jambo ambalo linaweza kuwavunja moyo.
“Kongamano hilo ni la kujadili na kutafuta suluhu ya matatizo tuliyonayo, tutumie tafiti za wanasayansi wa ndani badala ya kuwavunja moyo na kila anayejaribu kwa kutafiti apewe fursa ili aendelee kutafiti zaidi na matokeo tutayaona,” amesema.
Biteko amesema kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), serikali imetoa sh Bilioni 32 kwa ajili ya kuimarisha miradi ya utafiti na ubunifu.
Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia. Profesa Adolf Mkenda amesema Serikali imeanza kutambua jitihada za Wanasayansi, Watafiti wa ndani ya nchi na baadhi yao wametunukiwa vyeti kwa kutambua mchango wao kwa maendeleo yaliyofikiwa katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo na uvuvi.
Amesema njia moja ya kufanya jitihada hizo kuwa endelevu, Serikali imeanzisha mfuko wa mikopo nafuu wa kubiasharisha bunifu na tafiti Tanzania unaojulikana kama ‘Samia Fund’.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu ameishukuru Serikali kwa uwezeshaji ambao umeiwezesha kutekeleza majukumu yake kwa viwango na kuwa moja ya taasisi mahiri ya kupigiwa mfano Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Amesema COSTECH kupitia program mbalimbali imewasaidia vijana wengi kubadili ndoto zao kuwa fursa ambapo pamoja na mambo mengine imefikia uwezo wa kutoa vibali 1000 kwa watafiti kutoka nje ya nchi.
Balozi wa Norway nchini, Tine Tonnes ameipongeza Tanzania kwa hatua zake za kuendeleza watafiti na wabunifu huku akieleza utayari wa nchi hiyo kuendelea kuunga mkono program za uhifadhi wa mazingira.

You Might Also Like

Zitumieni fursa za misitu na nyuki-Tafori

Samia Asema Mwanamke Anayo Haki Ya Kumiliki Ardhi

Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika

Serikali Kupeleka Umeme Maeneo Ya Kimkakati

Dkt. Ndumbaro : Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Imefanikiwa 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Aongoza Waombolezaji Kutoa Heshima Za Mwisho Kwa Mbunge Ndungulile
Next Article REA Yaupamba Mkutano Wa Kikanda Wa Nishati Bora 2024
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Shinyanga Kunufaika Na Miradi Ya REA,Wauziwa Mitungi 13,000 Kwa Ruzuku
Habari June 2, 2025
SUA Chatumia Ngamia Mafunzo Ya Vitendo Kwa Wanafunzi
Habari June 2, 2025
Mama Mchumgaji TAG Zinga, Asheherekea Siku Ya Kuzaliwa Na Watoto Yatima, Mazingira Magumu
Habari June 2, 2025
CCCC Yaandaa Tamasha La Dragon Boat
Habari June 2, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?