MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Washauri Somo la Astronomia Kurudishwa Mashuleni, Kukuza Utalii Anga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Washauri Somo la Astronomia Kurudishwa Mashuleni, Kukuza Utalii Anga
Habari

Washauri Somo la Astronomia Kurudishwa Mashuleni, Kukuza Utalii Anga

Author
By Author
Share
3 Min Read
Baadhi ya vifaa maalumu ‘viona mbali’ kwa ajili ya ajili ya mafunzo ya elimu ya anga vilivyotumika katika mfumo ya utalii wa anga
Na Vincent Mpepo
ARUSHA: WATAALAMU wa elimu na utalii wametoa wito kwa mamlaka husika kulirejesha somo la Elimu ya Anga (Astronomia) katika mtaala wa shule za sekondari, ili kuwapata wataalamu zaidi watakaokuza sekta mpya ya utalii wa anga nchini.
Wito huo umetolewa na Mhadhiri Mwandamizi wa Fizikia na mtaalamu wa astronomia kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dkt. Noorali Jiwaji, wakati wa mafunzo ya biashara ya utalii wa anga yaliyofanyika mjini Karatu, mkoani Arusha.
“Nashangaa tutawapata wapi wanafunzi wenye msingi wa astronomia kama mtaala wa elimu wenyewe umelitupilia mbali somo hili muhimu,” amesema Dkt. Jiwaji.
Habari Picha 9483
Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya utalli wa anga wakifuatilia mafunzo hayo yaliyofanyika Karatu, Mkoani Arusha. (Picha na Vincent Mpepo).
Amesisitiza wakati Tanzania ikilenga kuanzisha utalii wa anga kama sekta mpya ya kiuchumi, ni muhimu elimu ya astronomia ikapewa kipaumbele kuanzia ngazi za chini za elimu.
Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa OUT mstaafu, Profesa Elifas Bisanda, ametoa rai kwa serikali kuanzisha somo la utalii wa anga kuanzia shule za msingi ili kuwaandaa mapema wataalamu wa baadaye.
“Utalii wa anga ni eneo jipya lenye fursa nyingi kwa nchi yetu. Ili kunufaika, tunahitaji kuanza mapema kuwaandaa wataalamu kupitia elimu rasmi,” amesema Bisanda.
Aidha, amewataka washiriki wa mafunzo kujiunga na mtandao wa  Anga-Giza (DarkSky – Tanzania) ili kukuza ushirikiano wa kitaalamu.
Naye Rais wa Chama cha Kimataifa cha Anga-Giza (International Dark-Sky Association) kutoka New Zealand, Nalayini Davis, amesema Tanzania ina nafasi ya kipekee katika kukuza utalii wa anga kutokana na mazingira bora ya asili, hali nzuri ya hewa na mandhari ya kuvutia.
“Ni wakati muafaka kwa Tanzania kuwekeza katika utalii wa anga kutokana na anga lenye giza safi na mandhari bora zinazotupa faida ambazo hazipaswi kupuuzwa,” amesema Davis.
Mafunzo hayo yaliandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwa kushirikiana na OUT, yakifadhiliwa na wataalamu kutoka New Zealand na Marekani, na yalihudhuriwa na wadau wa utalii wakiwemo waongoza watalii, watoa huduma za utalii, watunga sera, watafiti na wanataaluma zaidi ya 70.

You Might Also Like

NCCR-MAGEUZI Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 

Wanafunzi Wawili Wajiteka Ili Wapate Pesa Toka Kwa Wazazi wao

Hatuwezi Kukwepa Matumizi Ya Bioteknolojia – Dkt.Nguvila

Kipaji pekee hakitoshi katika kufanya kazi za kihabari – Kipangula

Washauriwa Kutumia Mbegu Zinazokabiliana Na Mabadiliko Ya Tabia Nchi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Dkt. Biteko Aahidi Kuendeleza Miradi Mikubwa Bugelenga
Next Article Majaliwa Kufungua Maonesho Ya Madini Geita Leo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?