MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wananchi Washauriwa Kujiunga Na Chuo Cha Ualimu Na Ufundi Stadi Morogoro
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wananchi Washauriwa Kujiunga Na Chuo Cha Ualimu Na Ufundi Stadi Morogoro
Habari

Wananchi Washauriwa Kujiunga Na Chuo Cha Ualimu Na Ufundi Stadi Morogoro

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

MOROGORO: KATIKA kuhakikisha taifa linakuwa na wataalamu mahiri katika sekta ya ufundi stadi, serikali kupitia Chuo cha Ualimu na Ufundi Stadi Morogoro (MVTC) imepanua wigo wa utoaji wa mafunzo ya ualimu wa ufundi, huku dirisha la udahili kwa mwaka huu likiwa wazi hadi mwisho wa mwezi Septemba.

Akizungumza na vyombo vya habari, Mkufunzi Mwandamizi wa chuo hicho, Rodgers Sabuni, amesema chuo hicho ndicho pekee nchini kilichopewa dhamana ya kitaifa ya kuwaandaa walimu wa kufundisha vyuo vya ufundi stadi vya serikali na binafsi.

“Huwezi kuwa mwalimu wa ufundi bila kupita kwenye mafunzo ya ualimu,” amesema Sabuni na kufafanua kuwa mafunzo yanayotolewa yanazingatia mbinu bora za kufundisha kwa vitendo, sambamba na miongozo ya serikali kuhusu uboreshaji wa elimu ya ufundi.

Amesema MVTC kwa sasa inatoa kozi tatu kuu ambazo ni Astashahada ya Uzamili ya Ualimu wa Ufundi Stadi Kwa wahitimu wa shahada ya kwanza ya uhandisi.

“Hii huwaandaa kufundisha walimu wa vyuo vya ufundi,” amesema.

Pia Cheti cha Walimu Wasaidizi wa Ufundi Kwa wahitimu wa ngazi ya vyeti kutoka vyuo kama VETA, wanaopata mafunzo ya mwaka mmoja katika mbinu za kufundishia kwa vitendo, hasa katika fani za karakana.

Vile vile Diploma ya Ualimu wa Ufundi katika Uhandisi, kozi mpya zinazolenga kuandaa walimu wa ufundi kwa mahitaji mapana ya sasa ya kitaifa.

Katika jitihada za kuleta usawa na kuwafikia Watanzania wengi, Sabuni amesema kuwa chuo hicho hutoa elimu kwa njia mbili ya masafa na ya ana kwa ana ili kuwawezesha hata wale walioko mbali kupata fursa hiyo adhimu.

Sabuni amesema mabadiliko ya sera ya elimu yamefungua milango mipana ya ajira kwa walimu wa ufundi, kwani shule nyingi za sekondari zinaanzisha mchepuo wa masomo ya ufundi huku serikali ikiendelea kujenga vyuo vya VETA katika kila wilaya.

“Hii ni fursa ya kipekee kwa vijana waliomaliza kidato cha nne, vyuo vya ufundi au vyuo vikuu kujiunga na mafunzo haya ambayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kuendeleza uchumi wa viwanda nchini,” amesema Sabuni.

Amesema kutokana na mahitaji makubwa ya walimu wa ufundi nchini, MVTC inatoa wito kwa vijana wote wenye nia ya kujihusisha na ualimu wa ufundi kuchangamkia dirisha la udahili lililofunguliwa kuanzia mwezi Juni hadi Septemba mwaka huu.

Kwa mujibu wa Sabuni, wahitimu wa mafunzo hayo hupata nafasi kubwa ya ajira katika sekta ya elimu ya ufundi na teknolojia, sambamba na kuwa chachu ya maendeleo katika jamii zao.

“Tunaandaa walimu wa ufundi si kwa ajili ya vyuo vya VETA tu, bali pia kwa shule za sekondari zinazotekeleza mchepuo wa ufundi. Hii ni nafasi ya kipekee kwa vijana wetu kushiriki katika ujenzi wa taifa kupitia taaluma hii ya kipekee,” amehitimisha.

You Might Also Like

Februari Mwaka Huu Wafanyabiashara Kariakoo Kurejea, Wenye Madeni Waagizwa Kulipa

Majaliwa Ataka Yatolewe Mafunzo Yanayozingatia Soko La Ajira

Wakulima wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea

Ndunguru: Mabadiliko Ya Tabianchi Yanachangia Kuwepo Kwa Magonjwa, Wadudu Kwenye Mazao

Miradi ya maedeleo na Huduma za afya isimamiwe kwa ukaribu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Singida Yapokea Zaidi Ya Milioni  Moja 
Next Article Mradi wa Maadili Katika Utafiti Wa Binadamu Na Huduma Za Afya Wafanywa UDSM kwa Ushirikiano wa Kimataifa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TSB Yatangaza Fursa Za Kilimo, Uwekezaji Wa Mkonge
Habari July 6, 2025
Elimu Ya Dawa Za Kulevya Kutolewa Kwa Wanafunzi
Habari July 6, 2025
Posta Yaleta   Usafiri Wa Kitalii Ndani Ya Sabasaba
Habari July 6, 2025
Mradi wa Maadili Katika Utafiti Wa Binadamu Na Huduma Za Afya Wafanywa UDSM kwa Ushirikiano wa Kimataifa
Habari July 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?