MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa
Habari

Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHUO Kikuu cha Dar es Salaam ( UDSM), kinajadili na kuchambua masuala yanayogusa dini, utamaduni na siasa ili kujenga misingi ya maelewano, heshima na mshikamano katika jamii.

Mhadhiri Msaidizi kutoka Idara ya Falsafa na Taaluma za Dini, Valeri Mujuni amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa habari hizi katika banda la chuo hicho lililopo katika maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Amesema pia katika maonesho hayo wanaeleza wananchi, kuhusu mradi huo unaolenga kuchochea mjadala wa kina kuhusu nafasi ya dini na utamaduni katika jamii ya sasa.

Amesema Mradi huo, unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU), unalenga kufanya tafiti zinazochambua mitazamo tofauti kuhusu masuala ya kidini ambayo kwa muda mrefu hayajapewa utafiti wa kina, huku ukilenga kuibua majibu mbadala kwa changamoto zinazojitokeza katika jamii.

“Tumejikita katika kufanyia kazi maeneo ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakionekana kuwa nyeti, kama vile ukinzani kati ya dini na siasa. Tunafahamu kuwa kuna mstari mwembamba unaotenganisha maeneo haya, na kwa sababu hiyo tunahitaji uelewa wa pamoja,” amesema Mujuni.

Amesema Mradi huo umekuwa jukwaa la wazi kwa wanafunzi na wataalamu kutoka nyanja mbalimbali kushiriki katika mashauriano, kubadilishana mawazo na kushirikiana kwa lengo la kukuza uelewa wa kijamii na kukuza misingi ya haki za binadamu kupitia falsafa na tafakuri ya kidini.

“Tunatumia falsafa kama chombo cha kuchambua kwa undani haki ya binadamu na namna tunavyoweza kuishi kwa kuheshimiana, kupendana na kujaliana licha ya tofauti zetu za kidini au kitamaduni,” amesema.

Kupitia ushiriki wao katika maonesho ya Sabasaba, amesema kwamba wanatoa picha ya mchango mkubwa wa taaluma ya dini katika kutatua changamoto za kijamii, huku wakisisitiza umuhimu wa tafiti shirikishi na mjadala wa wazi katika kujenga jamii yenye mshikamano na maelewano ya kweli.

You Might Also Like

Dodoma Yang’ara Katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani

Ujenzi Kiwanda cha Chumvi Waanza Lindi

Matumizi Mabaya Ya Dawa Husababisha Usugu Wa Vimelea Kwa Wanyama – Dkt. Kitimu

Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti

Vipaumbele Vilivyopo Kwenye Mpango Wa Maendeleo Vitafsiriwe – Majaliwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mama Janeth Magufuli Atembelea Banda La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba
Next Article
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?