MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanafunzi UDSM, MUM Kushiriki Fainali Ya Kimataifa Mashindano Ya Chinese Brigde
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanafunzi UDSM, MUM Kushiriki Fainali Ya Kimataifa Mashindano Ya Chinese Brigde
Habari

Wanafunzi UDSM, MUM Kushiriki Fainali Ya Kimataifa Mashindano Ya Chinese Brigde

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: HATIMAYE wanafunzi wawili wameibuka kidedea katika mashindano ya kuzungumza lugha ya Kichina, ‘ Chinese Bridge’ ambao watapata fursa ya kwenda nchini China kwa ajili ya fainali ya Kimataifa.
Mshindi maalum katika mashindano hayo ametoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Kuluthum Maftah ambaye atashiriki mashindano yatakayofanyika nchini China, huku mshindi wa kwanza kutoka Chuo Kikuu Cha Waislam Morogoro  (MUM), Sara mfinanga atapata nafasi ya kwenda kuyashuhudia.
Akizungumza wakati wa mashindano yaliyofanyika UDSM, Rasi wa Ndaki ya Insia, chuoni hapo Dkt. Silkiluwasha Mpale ambaye amemwakilisha  Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa William Anangisye amesema mashindano hayo ya ” Chinese Bridge yanahusisha  vipaji mbalimbali kutoka kwa washiriki wake.
Amesema mashindano hayo ni ya 24 ya umahiri wa Lugha ya Kichina na ya 12 kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Tanzania.
Amesema lengo la mashindano hayo ni kuthamini ujuzi wa wanafunzi katika stadi mbalimbali za lugha ya kichina na tamaduni zake.
” Miongoni mwa maeneo yanayotazamwa ni utoaji wa hotuba, uimbaji wa nyimbo, kughani mashairi na Sanaa mbalimbali ikiwa ni pmoja na uchoraji,” amesema.
Pia amesema taasisi ya kufundisha lugha ya Kichina ya Confucius imeanza kutoa mafunzo ya lugha ya kiswahili kwa wachina wanaoishi nchini Tanzania.
“Wachina hawa wamependa kufundishwa na walimu wanaofahamu lugha na utamaduni wa Kichina. Kwa kufanya hivi tunakamilisha msemo wa nipe nikupe.
” Kwa maana kwamba sisi tunajifunza lugha na utamaduni wa Kichina, wakati huo huo wachina wanajifunza lugha na utamaduni wa Kiswahili,” amesema.
Mkurugenzi Mtanzania wa Confucius Dkt. Mussa Hans, amesema kwamba mashindano hayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 na hufanyika katika hatua mbili.
“Hatua ya kwanza hufanyika katika nchi mbalimbali ulimwenguni , hatua ya pili ni fainali ya kimataifa ambayo hufanyika nchini China.
” Hadi sasa zaidi ya wanafunzi milioni 1.5 kutoka zaidi ya nchi 150 wamekwishashiriki mashindano haya na kuonesha mafanikio makubwa katika kujifunza kwa kichina.
“Zaidi ya washindi 5000 wamekwishasafirishwa kwenda China kushiriki mashindano ya fainali ya kimataifa,” amesema.
Amesema lengo la mashindano hayo ni kutoa jukwaa kwa washiriki kutoka maeneo mbalimbali  kuonesha ustadi wao wa lugha ya kichina, kujenga mtandao baina yao  na kuhamasisha kufanya bidii zaidi katika kujifunza lugha na utamaduni wa kichina.
“Taasisi yetu ya Confucius pia imedhamiria kuwa daraja baina ya wahitimu wa mafunzo ya kichina na makampuni mbalimbali kwa lengo la kutafuta fursa mbalimbali,” amesema.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Balozi wa China nchini, Wang Yong amesema kushiriki kikamilifu katika shindano hilo kwa wanafunzi wa Kitanzania kunaonyesha nia, shauku na matarajio  ya vyuo vya Tanzania, wazazi na wanafunzi katika kujifunza lugha hiyo na kuelewa utamaduni wake.
“Ubalozi wa China unatumai kuwa mashindano hayo yatakuwa faraja na jukwaa la kukuza ufundishaji na ujifunzaji wa Kichina nchini Tanzania,
“Pia kukuza mawasiliano ya kitamaduni baina ya nchi hizi mbili ” amesema.

You Might Also Like

Utiaji Saini Mkataba Wa Ujenzi Jengo La TUGHE Wafanyika

Matwebe Aipongeza Serikali Kushirikisha JUMIKITA  Kwenye Shughuli Za Kitaifa

Rais Wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Mgeni Rasmi Mkutano Wa THRAPA

Masauni Kuzifanyia Kazi Changamoto Alizozibaini Katika Ziara Yake

Chagueni Viongozi Wanaofaa-Biteko

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article JAB Yaanza Rasmi Kutoa Vitambulisho Kwa Waandishi Wa Habari
Next Article Polisi Dodoma Yawataka Wananchi Kutoa Taarifa 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Dkt. Ndumbaro : Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Imefanikiwa 
Habari May 20, 2025
Senyamule Ahamasisha Ushiriki Wa Vijana Katika Uchaguzi
Habari May 20, 2025
Polisi Dodoma Yawataka Wananchi Kutoa Taarifa 
Habari May 20, 2025
JAB Yaanza Rasmi Kutoa Vitambulisho Kwa Waandishi Wa Habari
Habari May 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?