MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wafanyakazi Majumbani Walia: ‘Tunaishi Katika Mazingira Hatarishi’
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wafanyakazi Majumbani Walia: ‘Tunaishi Katika Mazingira Hatarishi’
Habari

Wafanyakazi Majumbani Walia: ‘Tunaishi Katika Mazingira Hatarishi’

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MOROGORO: WAFANYAKAZI wa majumbani wameiomba Serikali kukamilisha haraka mchakato wa kuridhia Mkataba Na. 189 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), kwa kuwa ucheleweshwaji huo unaendelea kuwaumiza kwa kufanya kazi katika mazingira yasiyo na staha wala ulinzi wa kisheria.
Wakizungumza kwenye kikao kazi cha mafunzo ya utatuzi wa migogoro kilichofanyika mjini Morogoro, wafanyakazi hao walieleza kuwa wengi wao hawana mikataba rasmi ya kazi, wanakosa mapumziko, haki ya faragha, na kinga ya kisheria.
“Wafanyakazi wa majumbani tunatakiwa kutambua haki, stahiki pamoja na sheria za haki na wajibu,” amesema Desdelia Saimon kutoka Morogoro,.
Amesema kuchelewa kuridhiwa kwa mkataba huo kunawafanya waendelee kufanya kazi katika mazingira hatarishi.
Naye Nasra Selemani kutoka Dar es Salaam amesema mkataba huo ukiidhinishwa utafungua fursa nyingi kwa wafanyakazi wa majumbani.
“Tunamuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuridhia mkataba huu ili na sisi tutendewe haki kama wafanyakazi wengine,” amesema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wafanyakazi wa Majumbani Tanzania, Zanini Athuman, amesema mkataba huo unaweka wazi stahiki halali kwa kundi hilo, ikiwa ni pamoja na mapumziko ya kutosha na mazingira ya kuishi kwa heshima kwa wale wanaoishi kwa waajiri.
Amesema licha ya sheria za kitaifa kutambua kundi hilo, utekelezaji wake unakuwa mgumu kutokana na nyumba ya mtu binafsi kutotambulika kama eneo rasmi la kazi.
Katibu Mkuu wa CHODAWU, Said Wamba, amehimiza wafanyakazi wa majumbani kujiunga na vyama vya wafanyakazi ili wawe na sauti ya pamoja katika kudai haki na stahiki zao.
“Tunajaribu kuwainua hawa wafanyakazi wa majumbani. Wapo chini mno na hili si jukumu la CHODAWU pekee, bali jamii nzima inapaswa kushiriki kuwaokoa,” amesema.
Kwa mujibu wa Wamba, wafanyakazi hao hufanya kazi kubwa na muhimu kwa waajiri wao na taifa kwa ujumla, lakini hawapati matunda ya jasho lao.
Pia Mratibu wa mradi wa ILO, Chiku Semfuko, amesema mafunzo hayo yatawawezesha wafanyakazi wa majumbani kufahamu mahali sahihi pa kupeleka migogoro yao na namna ya kupata utatuzi.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa CMA Tanzania Bara, Usekelege Mpulla, amesema tume imekwishaandaa mwongozo maalumu wa kushughulikia migogoro ya wafanyakazi wa majumbani pekee kwa lengo la kutafsiri matakwa ya kisheria na mkataba namba 189.
“Tumejipanga kuhakikisha haki za wafanyakazi wa majumbani zinatolewa kwa wakati, na mafunzo haya yatawajengea uwezo wasuluhishi kumaliza migogoro kwa haraka,” amesema.
Akifungua mafunzo hayo, Kamishna Msaidizi wa Idara ya Kazi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Rehema Moyo amesisitiza kuwa CMA inapaswa kutoa kipaumbele kwa migogoro ya wafanyakazi wa majumbani kutokana na ugumu wa mazingira wanayopitia.
“Ni muhimu hata wao wafahamu haki zao. Hata kama vyombo vipo, lazima wapewe elimu ya kujua wapi waende kupata suluhu ya migogoro yao,” amesema Moyo.
Katika kuhakikisha haki za wafanyakazi wa majumbani zinalindwa ipasavyo, Shirika la Kazi Duniani (ILO) limewakutanisha mkoani Morogoro Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), taasisi zinazohusika na migogoro ya kazi, pamoja na wawakilishi wa wafanyakazi wa majumbani kwa lengo la kutafuta suluhu ya pamoja

You Might Also Like

Rais Mwinyi Ajionea Mifumo Mbalimbali Banda La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba

TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi

COSOTA Yapokea Migogoro 136 Ndani Ya Miaka Minne

Kanisa La GCC Kufanya Maombi Kuelekea Uchaguzi Mkuu

Samia ashiriki mashindano ya dunia ya Quran

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TASAC Yashuhudia Utiaji Saini  Mkataba Wa Uendeshaji Bandari Kavu Kwala
Next Article Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Wajitosa Kugombea Ubunge
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Habari August 1, 2025
Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi
Habari August 1, 2025
Rais Samia Aipa Neema Miradi Ya Kuzalisha Umeme Iringa
Habari August 1, 2025
Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini
Habari July 31, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?