MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Yawawezesha Vijana Wenye Mahitaji Maalum Kung’ara Katika Fani za Ufundi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Yawawezesha Vijana Wenye Mahitaji Maalum Kung’ara Katika Fani za Ufundi
Habari

VETA Yawawezesha Vijana Wenye Mahitaji Maalum Kung’ara Katika Fani za Ufundi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: Balozi wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) katika Kitengo cha Watu Wenye Mahitaji Maalum, Francis Anthony, amesema anachukia kuonavwenye mahitaji maalum wakiwa ombaomba hivyo anawahamasisha kujifunza ujuzi mbalimbali utakaowasaidia katika maisha yao.
Anthony amesema hayo mbele ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. Mary Maganga, alipotembelea banda la VETA katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana yanayoendelea mkoani Mbeya.
Habari Picha 9826
Akimwelezea Katibu Mkuu huyo, Maganga amesema kwamba ni mhitimu wa VETA,  fundi wa kompyuta aliyehitimu mafunzo ya kitaalamu na sasa anafundisha wengine.
Amesema uwepo wake katika maadhimisho hayo ni kuhamasisha vijana wenye ulemavu wasikate tamaa bali wajitokeze kupata mafunzo ya ufundi ili waweze kujitegemea kama wenzao.
“Nilianza kama mwanafunzi, sasa ninafundisha. Huu ni uthibitisho kuwa VETA imewajengea uwezo vijana wenye mahitaji maalum, na hata sisi tuna ujuzi wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa,” amesema.
Habari Picha 9827
Kwa upande wake, Riziki Ndumba, mwanafunzi wa VETA Songea anayesomea fani ya ushonaji, amesema alianza bila kuwa na ujuzi wowote wa awali, lakini kupitia mafunzo aliyopata na msaada kutoka kwa walimu pamoja na viongozi wa chuo, ameweza kumaliza kozi ya miaka miwili kwa mafanikio.
“Lengo langu ni kuonyesha kwa vitendo kuwa hata sisi wenye ulemavu tunaweza kufanya kazi na kujitegemea kama vijana wengine. Nawashukuru VETA kwa kutuamini na kutuwezesha,” amesema.
Habari Picha 9828
Naye Ofisa Uhusiano kwa Umma VETA Makao Makuu, Elmer Sarao, ameeleza kuwa taasisi hiyo inaendelea kutoa nafasi kwa vijana wenye ulemavu katika vyuo vyake.
Amesema mmoja wa walimu waliopo sasa ni mhitimu mwenye ulemavu aliyesoma VETA kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa tatu, na sasa anafundisha katika chuo cha mafunzo stadi kilichopo Morogoro.
“Huyu ni mfano hai kuwa ulemavu si kikwazo cha ufanisi. Tunajivunia kuwalea na kuwaendeleza vijana hawa,” amesema.
  • Habari Picha 9829
Amesema VETA imekuwa ikitoa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana wa makundi yote, ikiwemo wenye mahitaji maalum, kama sehemu ya juhudi za serikali katika kujenga taifa lenye nguvu kazi mahiri na jumuishi.

You Might Also Like

Rais Samia afurahia SGR

Mtoto Wa Miaka Sita Ashinda Ashindano Ya Kuhifadhi Quraan Mkoa Arusha

TTCL Yafanya Maboresho Makubwa Kwa Watumiaji

Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato

Sagini Amwelezea Kaluta Amir Abeid Ni Alama Ya Kuigwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sekta ya Huduma Kuchangia Asilimia 45 Katika Uchumi Wa Nchi
Next Article TUCTA Yaitaka Jamii Kuwapa Nafasi Vijana Wenye Changamoto za Kimwili
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?