MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA kushirikiana na Toyota Tanzania kuboresha mafunzo ya ufundi magari
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA kushirikiana na Toyota Tanzania kuboresha mafunzo ya ufundi magari
Habari

VETA kushirikiana na Toyota Tanzania kuboresha mafunzo ya ufundi magari

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imepanga kuimarisha ushirikiano na Toyota Tanzania Limited kwa ajili ya kuboresha mafunzo ya ufundi magari kwa wakufunzi na wanafunzi wa vyuo vya VETA.
Hayo yameelezwa katika ziara ya Menejimenti ya VETA ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Anthony Kasore, iliyoambatana na wataalam kutoka Makao Makuu ya VETA, Kanda ya Dar es Salaam, Chuo cha VETA Dar es Salaam na walimu wa vyuo vya Dar es Salaam na Pwani, iliyofanyika Agosti 12, mwaka huu 2025 katika ofisi na karakana za Toyota Tanzania, jijini Dar es Salaam.
Habari Picha 8861
Kasore amesema lengo la ziara ni kujifunza kuhusu teknolojia mpya, mifumo ya matengenezo ya magari ya Toyota na namna kampuni hiyo inavyowawezesha mafundi kuwa mahiri.
Amesema VETA inakusudia kushirikiana na Toyota kutoa mafunzo ya kuongeza umahiri kwa wakufunzi na wanafunzi wa fani za magari.
“Magari ya Toyota yanatumika kwa kiwango kikubwa nchini, hivyo ni muhimu wakufunzi na wanafunzi wetu wawe na uelewa wa kina ili wafanye matengenezo bora,” amesema.
Meneja Mkuu wa Toyota Tanzania, Kadiva William, amepongeza hatua hiyo akisema, “VETA mnazalisha tunachokitumia, na sisi tunatoa huduma mnayoitumia, hivyo tunategemeana.”
Mkuu wa Shughuli za Usambazaji wa Toyota, Stanley Joseph, amesema ushirikiano huo utarahisisha utoaji wa mrejesho kuhusu wahitimu wa VETA na kufuatilia mabadiliko ya teknolojia, yakiwemo magari yanayotumia gesi na mafuta.
Habari Picha 8862
Mkufunzi wa Toyota, Michael Mruma, amesema kampuni hiyo ina chuo maalum kinachotoa mafunzo ya umakenika, umeme wa magari, urekebishaji bodi, huduma kwa wateja, usimamizi wa vifaa na mbinu za Kaizen. Ametoa wito wa kuunganisha mafunzo ya umakenika na umeme wa magari badala ya kuyatenganisha kama ilivyo sasa katika vyuo vya VETA.
Pande zote zimekubaliana kurasimisha ushirikiano ili kuhakikisha mafunzo yanalingana na mahitaji ya soko la ajira na kuinua viwango vya wakufunzi.
Kasore amesema VETA itaandaa andiko la mapendekezo ya kurasimisha ushirikiano huo.
Toyota kwa sasa inatoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa VETA katika vituo vya Dar es Salaam, Tanga na Arusha.

You Might Also Like

Ridhiwani, Waziri Wa Kazi, Ajira UAE Waweka mkakati

Waziri Ridhiwani Akutana Na Balozi Wa Japan Nchini,  Wazungumzia Vijana

CATC yawaita wakulima kusomea urushaji wa ndege nyuki

Bodi ya mkonge kutoa ajira kwa watu 10,000 ifukapo 2030

Rais Samia ashuhudia JOWUTA Ikiwa mwanachama wa  TUCTA 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article SADC Yasisitizwa Kuhusu Safari ya Ukombozi wa Kiuchumi
Next Article SADC, Marekani Kuanzisha Jukwaa La Majadiliano
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?