MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Uvuvi Wa Kisasa Wainua Mwanza Kiuchumi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Uvuvi Wa Kisasa Wainua Mwanza Kiuchumi
Habari

Uvuvi Wa Kisasa Wainua Mwanza Kiuchumi

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
Dodoma: MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda amesema matumizi ya teknolojia ya kisasa yamechochea mageuzi makubwa katika sekta ya uvuvi mkoani humo, na kuifanya Mwanza kuwa kinara katika uchakataji, usafirishaji na ufugaji wa samaki nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita, Mtanda amesema mkoa huo umevuna matunda ya uwekezaji katika teknolojia ya uzalishaji na usindikaji wa mazao ya samaki, hatua inayochochea uchumi wa buluu na kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.
“Idadi ya vizimba vya kufugia samaki imeongezeka kutoka 1,664 mwaka 2020 hadi kufikia 2,715 mwaka 2025. Ni mafanikio makubwa ya uwekezaji katika teknolojia ya kisasa ya ufugaji wa samaki,” amesema.
Kwa mujibu wa Mtanda, mwaka 2024 pekee zaidi ya tani 43,657.6 za minofu ya samaki zilichakatwa, huku tani 81,812 zikisafirishwa nje ya nchi kupitia Uwanja wa Ndege wa Mwanza.
Pia, usafirishaji wa mabondo ya samaki nje ya nchi umeongezeka kutoka kilo 431,721 mwaka 2020 hadi kilo 495,448 mwaka 2024.
Amesema Idadi ya mabwawa ya kufugia samaki pia imepanda kutoka 286 mwaka 2020 hadi 531 mwaka 2025, ongezeko la zaidi ya asilimia 85.
 “Mapato ya shughuli za uvuvi mkoani Mwanza yameongezeka kutoka Sh. Bilioni 4.4 mwaka 2020 hadi Bilioni 8.2 mwaka 2025.
“Haya ni mafanikio ya moja kwa moja ya sera na msukumo wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kukuza uchumi wa buluu,” amesema.
Mkuu huyo wa mkoa amesema Mwanza itaendelea kuhamasisha uwekezaji, utafiti na matumizi ya teknolojia, ili kuhakikisha kuwa rasilimali za Ziwa Victoria zinawanufaisha wavuvi wadogo, wanawake, vijana na wafanyabiashara wa dagaa kwa uendelevu.

You Might Also Like

Rais Samia Azindua Makao Makuu Ya Mahakama Tanzania

Madereva Mabasi YA Kukodi Waitwa LATRA Kabla YA Januari 12, Mwaka Huu

VETA Mtwara Yawafundisha Wanafunzi Uongezaji Thamani Kwenye Korosho, Mwani

Waajiri Wasilisheni Michango Kwa Wakati

Waziri wa Vijana akutana na Mwita wa Zanzibar

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tanzania Yaingia Saba Bora Duniani  Kwa Uzalishaji Wa Pamba Hai
Next Article CCM Yasitisha Ratiba ya Uchaguzi wa Maoni
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CCM Yasitisha Ratiba ya Uchaguzi wa Maoni
Habari July 19, 2025
Tanzania Yaingia Saba Bora Duniani  Kwa Uzalishaji Wa Pamba Hai
Habari July 19, 2025
Mara Yapaa: Miaka Minne Ya Mafanikio Chini Ya Rais Samia
Habari July 18, 2025
Serikali Yazindua Mafunzo Ya Mtandao Ya Afya Moja
Habari July 16, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?