Na Lucy Lyatuu
DODOMA: SERIKALI imepokea ndege mpya ya Kisasa ya kudhibiti visumbufu vya mimea nchini aina ya Trash P2+ na kuagiza mchakato Wa ununuzi Wa ndege nyingine tatu kuanza mara Moja kwa vituo vingingine nchini kuanzia sasa.
Waziri Wa Kilimo Hussein Bashe amesema hayo wakati akipokea ndege hiyo jijini Dodoma, iliyoingia kwa uratibu wa Mamlaka ya Afya Ya Mimea Na Viuatilifu Tanzania {TPHPA).
Akizungumza ametoa maelekezo kwa Mamlaka hiyo kuhakikisha katika vituo vinne vya Kilimo nchini kuwe na Kilimo anga vikiwa na ndege pamoja na drones na mchakato Wa ununuzi Wa ndege hizo uanze sasa.
Amesema mchakato Wa ununuzi Wa ndege hizo uanze akiwa Bado madarakanu kabla ya kwenda kwenye Uchaguzi Mkuu kwa kuwa bajetibya Kilimo imeshapita.
“Ni lazima kama nchi tujitegemee,dunia ya kubebana haipo,wadau Wa maendeleo tunawashukuru sana,” amesema Bashe akitaja vituo vinne vya Kilimo kuwa ni Arusha, Dodoma,Mwanza na Mbeya.
Amesema kama nchi imeshaanza kununua drones kwa ajilibya ufuatiliaji na sasa inanunuankwa ajilibya kunyunuiza na hivyo lazima watanzania wajue hilo.
Bashe amesema knunuliwa kwa ndege hiyo ni kupanua wigo Wa umwagiliahi na KWAMBA Kila Miundombinu inayoongezwa ya umwagiliahi ni kukaribisha kweleakwelea.
“Hivyo kelele za kwelea kwelea ni nchi nzima na kwamba Ilani ya ChamanCha Mapinduzi (CCM) iliyozinduliwa inazungumzia Kuwekeza kwenye Kilimo Cha umwagiliaji,” amesema na kuongeza kuwa ndio maana Kuna Mradi mkubwa Wa umwagiliaji kwa ziwa Viktoria na Tanganyika wenye hekta milioni tatu.
Amesema hivyo lazima kujiandaa, na kutambua kuwa Tanzania ina maeneo yenye mazalia ya nzige wekundu ambayo ni Dodoma,Katavi na Rukwa.