MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ulega: Miaka 50 ya ILRI imeinufaisha Tanzania 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ulega: Miaka 50 ya ILRI imeinufaisha Tanzania 
Habari

Ulega: Miaka 50 ya ILRI imeinufaisha Tanzania 

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Mifugo (ILRI), imekuwa ikisaidia maendeleo ya sekta ya kuku nchini kupitia miradi rasmi na ile isiyo rasmi katika kuwajengea uwezo na kuwawezesha wanawake na vijana.

ILRI imekuwa ikiwezesha wanawake na vijana kwenye ujasiriamali wa lishe bora unaowawezesha kuwaongezea kipato.

Ulega amesema hayo wakati wa hafla ya kutimiza miaka 50 toka kuanzishwa kwa tasisi hiyo.

Amesema kwa uwezeshaji huo wa ILRI kwa wanawake na vijana umewezesha kuwepo kwa ushirikiano katika mnyororo wa thamani wa ufugaji huo wa kuku, katika kutafuta namna ya  kuimarisha ushindani wa wakulima katika eneo la lishe bora.

Amesema kampeni iliyoongozwa na ILRI na wadau wengine iliwezesha upatikanaji wa mifugo bora ya kuku inayoweza kukabiliana na magonjwa  na ufugaji wenye tija.

“Asilimia 65 ya wanawake wafugaji wa kuku wa mkoani Kilimanjaro na Lindi walipata uzoefu wa namna ya kudhibiti magonjwa ya kuku, hali iliyowafanya kuongezeka kwa mifugo, kuongezeka kwa kipato na kuwa na familia bora,” amesema.

Amesema katika kusherehekea miaka hiyo 50 kwa Tanzania kama nchi imenufaika na taasisi hiyo ambapo wizara yake imekuwa ikishirikiana moja kwa moja katika shughuli zake.

“Wizara ya Mifugo na Uvuvi inafanya kazi na wadau mbalimbali washirika wa maendeleo, wafadhili, sekta ya umma na binafsi, naweza kushuhudia

kwamba ILRI imekuwa mshirika mzuri katika maeneo mengi, ikiwa ni msaada mkubwa kwa wizara kwa kushirikiana na Taasisi ya Taifa ya Utafiti Tanzania, Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI).

“Mipango ambayo ILRI na washirika wake wamefanya kazi tangu uongozi wangu

kama naibu waziri wa mifugo na uvuvi hadi sasa

isiyoweza kuhesabika, lakini nitaonyesha mafanikio machache,” amesema Ulega.

Amesema mafanikio hayo ni pamoja na watumishi wa wizara yake kupata msaada wa kiufundi kutoka ILRI pamoja na msaada wa fedha kutoka kwa Bill na Melinda Gates mwaka 2016.

Pia amesema taasisi hiyo kwa kushirikiana na TALIRI wamesajili zaidi ya wanyama 69,000 kutoka makundi 33,000 mkoani Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Iringa,Njombe, Mbeya, na Songwe.

Vile vile amesema jitihada zilizofanywa na taasisi hiyo katika kuwashirikisha wanawake na vijana kumewezesha kutatua changamoto ya ajira hapa nchini.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mkuu eneo la Utafiti na Ubunifu wa Mifugo ya Kimataifa kutoka ILRI, Fabian Kausche amesema wamepata heshima kubwa kuweka alama ya utendaji wao kwa miaka 50 nchini Tnzania, ambapo taasisi hiyo ilikuwepo tokea mwaka 1997.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa ILRI, Appolinaire Djikeng, Kausche amesema Tanzania ina nafasi ya pekee kutokana na ushirikiano iliyonayo na taasisi hiyo.

Amesema mkakati mpya wa taasisi hiyo ni kuboresha

maisha ya watu milioni 300 kwa kuzingatia ufugaji endelevu wa kisayansi.

“Ili kufikia hili, tutafanya kazi katika maeneo manne yaliyounganishwa ambayo yanashughulikia mifugo

maendeleo na masuala mapana kama vile afya, hali ya hewa na mazingira.

“Pia tutaelekeza juhudi zetu kimkakati zaidi ndani ya nchi kwa kuweka kipaumbele kwa minyororo maalum ya thamani iliyotambuliwa na serikali na kufanya kazi na sekta binafsi, washirika wa maendeleo na watendaji wengine wasio wa serikali kuhakikisha wana mtazamo wa pamoja na endelevu,” amesema.

Amesema ili kufungua uwekezaji katika sekta wanahitaji kusaidia serikali kuweka sera wezeshi katika mazingira ya kukuza ukuaji.

“Hili ni eneo tunalofanyia kazi,na tuko tayari kushirikiana na kuongoza.

ILRI inapitia mabadiliko mengi ya ndani ili kuhakikisha kuwa tuko kimkakati

iliyounganishwa kufanya kazi na washirika na kutoa athari ambayo sote tunataka,” amesema.

You Might Also Like

Biteko Atoa Somo Uzalishaji Matumizi ya NIishati Afrika

Ridhiwani Kikwete Awataka Vijana Kuwa Mabalozi Wazuri wa Amani

Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Wanawake Jijini Arusha

Kikosi Kazi Maalumu Cha Kupitia Muongozo Wa Ufasili Wa Sheria Chazinduliwa

MOI Yaeleza Sababu Viungo Bandia Kuuzwa Kwa Bei Kubwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika
Next Article Waziri Mkuu Majaliwa Azungumzia Urushaji Wa Satelite Tanzania
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?