MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: UDSM Yapiga Hatua Kubwa Kuboresha Miundombinu na Mitaala kwa Mradi wa HEET
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > UDSM Yapiga Hatua Kubwa Kuboresha Miundombinu na Mitaala kwa Mradi wa HEET
Habari

UDSM Yapiga Hatua Kubwa Kuboresha Miundombinu na Mitaala kwa Mradi wa HEET

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
4 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa William Anangisye, amesema utekelezaji wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi (HEET) umefikia zaidi ya asilimia 80, na umeleta mageuzi makubwa katika miundombinu, mitaala, na teknolojia ya kufundishia chuoni hapo.

Profesa Anangisye amesema hayo alipokuwa akielezea kwa Wahariri na Waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa mradi huo.

Habari Picha 10107

Amesema chuo hicho ilitengwa dola milioni 49.5 (takribani Sh bilioni 121) kati ya dola milioni 425 zilizotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Pia amesema kupitia mradi huo, UDSM imejenga kampasi mpya katika mikoa ya Lindi na Kagera, majengo 11 mapya ya kufundishia na ofisi za wahadhiri, pamoja na hosteli za wanafunzi. Pia, miundombinu ya TEHAMA imeimarishwa, na sasa chuo kina uwezo wa kusambaza mtandao wa hadi 10Mbps kutoka 1.5Mbps.

Profesa Anangisye amesema zaidi ya mitaala 250 imeboreshwa ili kuendana na soko la ajira, na masomo 1,000 yamewekwa katika mfumo wa kujifunza kwa njia ya mtandao unaowawezesha wanafunzi 39,000, wakiwemo 165 wenye mahitaji maalum.

Habari Picha 10112

Katika kukuza utafiti na ubunifu, UDSM imesaini mikataba ya ushirikiano na kampuni 24 za sekta binafsi, jambo lililosaidia wahitimu kupata uzoefu wa kazi na kuongeza ajira.

Aidha, wanataaluma 29 wamefadhiliwa kusoma nje ya nchi, wakiwemo wanawake 13, katika shahada za Uzamili na Uzamivu, ili kuongeza ubora wa ufundishaji na utafiti.

Profesa Anangisye amesema mafanikio ya HEET yameongeza ubora wa elimu, ubunifu, ajira kwa wahitimu, na kuifanya UDSM kuwa kinara wa mageuzi ya kidijitali katika elimu ya juu nchini.

Ametoa shukrani kwa Serikali , Wizara ya Elimu, na Benki ya Dunia kwa kusaidia kufanikisha mradi huo.

“HEET ni ukurasa mpya katika historia ya elimu ya juu nchini. UDSM itaendelea kuwa chachu ya maendeleo kupitia falsafa yake — Hekima ni Uhuru.”

Habari Picha 10108

Naye Naibu Mratibu wa HEET chuoni hapo, Profesa Liberato Haule amesema kupitia mradi huo wamefanikiwa kuboresha miundombinu ya ufundishaji ikiwemo ujenzi wa majengo mapya, madarasa na maabara za kisasa.

Amesema mradi huo pia umeweka kipaumbele kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa kununua vifaa maalum vitakavyowawezesha kujifunza kwa urahisi pamoja na kurahisisha ufundishaji kwa walimu.

Habari Picha 10114

Kwa upande wa mageuzi ya mitaala, Profesa Haule anesema chuo kimepitisha mitaala 250 kupitia Seneti yake, ambapo 94 kati ya hiyo inatumika kupima matokeo ya mradi. Aidha, mitaala 32 imepata ithibati ya vyuo vikuu, miwili inatolewa kwa njia ya mtandao na 96 kwa mfumo wa mseto.

“Mabadiliko haya yanajibu kilio cha wadau wengi wanaotaka wahitimu wawe na ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira,” amesema Profesa Haule.

Habari Picha 10109

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, amepongeza serikali kwa kufadhili mradi huo na kuwashukuru wasimamizi kwa utekelezaji mzuri.

Amesema waandishi wa habari wataendelea kutangaza ubunifu na mafanikio ya UDSM ili kuvutia wawekezaji zaidi katika sekta ya elimu ya juu.

Habari Picha 10110

You Might Also Like

China Inaongoza Sekta ya Miundombinu na Ujenzi Tanzania

Mwanafunzi Wa Shule Ya Msingi Mbezi, Aokolewa Mikononi Mwa Mtekaji

TAWA Ni Mahali Sahihi Pa Uwekezaji  – Maganja

Majaliwa Aagiza Sera Ya Elimu Kusimamiwa Kikamilifu

Serikali Yaahidi Kupatia Dawa Kilio Cha Ushuru Kwa Malori

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Matukio Mbalimbali Ya Kampeni Za CCM Dar
Next Article MWALIM: Njaa na Ukosefu wa Ajira Ni Matokeo ya Uongozi wa CCM
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Kuja Na Mwongozo Wa Kuimarisha Ushirikishwaji Jamii Katika Masuala Ya Afya
Habari October 22, 2025
TUGHE Yatoa Wito Kwa Wafanyakazi Kujitokeza Kupiga Kura
Habari October 22, 2025
Mwalim Ahaidi Kubadilisha Dodoma Kuwa Jiji Kamili La Makao Makuu
Habari October 22, 2025
MWALIM: Njaa na Ukosefu wa Ajira Ni Matokeo ya Uongozi wa CCM
Habari October 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?