MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa ipo kwenye kilimo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa ipo kwenye kilimo
Habari

Theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa ipo kwenye kilimo

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi wetu, Nzega Tabora
SEKTA ya Kilimo inatajwa kuwa mhimili wa uchumi wa Tanzania, ikiajiri takribani theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa na kuchangia asilimia 65 ya malighafi za viwanda, asilimia 100 ya usalama wa chakula, na zaidi ya asilimia 26 ya pato la taifa.
Akizungumza katika mkutano na wakulima katika kijiji cha Ndala Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora, Mkuu wa Wilaya hiyo Naitapwaki Tukai amesema, maendeleo ya mwananchi na taifa yanategemea ufanisi katika sekta ya kilimo hivyo ni wajibu wa kila mkulima kuzingatia kanuni bora za kilimo ikiwemo matumizi sahihi ya mbolea.
Amesema  bajeti ya Wizara ya Kilimo kutoka bilioni 294 mwaka 2021/22 hadi trilioni 1.24 mwaka wa fedha wa 2024/25 ambapo lengo hasa ni kufanya mapinduzi katika Sekta ya Kilimo kwa kuongeza tija.
Aidha aliongeza kuwa Serikali imeendelea kutoa mbolea kwa bei ya ruzuku kwa misimu mitatu mfululizo,  kuhakikisha mkulima anapata mbolea kwa bei himilivu na kuwakumbusha wakulima kuitumia mbolea hiyo kwa usahihi ili ilete matokeo mazuri wakati wa mavuno.
“Tukipata matokeo mazuri wakati wa mavuno tutakua na uhakika wa chakula kwa mkulima mmoja mmoja, uhakika wa chakula kwa Taifa letu lakini pia tutapata ziada kwaajili ya biashara ili kukidhi mahitaji mengine ya familia”, aliongeza.
Naye mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt. Anthony Diallo alitumia wasaa huo kuwakumbusha wakulima kutumia mbolea sahihi, kwa wakati sahihi, kwa kipimo sahihi na eneo sahihi la mmea.
“Ndugu zangu wakulima leo tumekusanyika hapa ili tukumbushane kupitia kampeni yetu ya Kilimo Ni Mbolea tuone mabadiliko katika mavuno yetu kwa kuzingatia kanuni nne muhimu za matumizi sahihi ya mbolea ili tuendelee kupata mavuno mengi na bora”,alisema Dkt. Diallo.
Pamoja na hilo Dkt. Diallo aliwakumbusha wakulima kusajiliwa kwenye daftari la wakulima na kuingia kwenye mfumo wa kidigitali wa mbolea ya ruzuku ikiwa ni moja kati ya hatua muhimu kwa uzalishaji tija na ukuaji wa sekta ya Kilimo nchini.
“Kwasababu Kilimo ni Mbolea hatuna budi kuchangamkia fursa ya usajili tukiwa na kitambulisho cha NIDA au cha mpiga kura baada ya hapo tutumie mbolea kwa kuzingatia kanuni nne muhimu za mbolea ambazo ni nunua mbolea sahihi, tumia mbolea kwa wakati sahihi, kwa kipimo sahihi na sehemu sahihi, kwa kuzingatia hayo tutaendelea kuneemeka kwa chakula na kipato pia”, alibainisha Dkt. Diallo.
Vilevile Dkt. Diallo aliongeza kuwa kwa kusajiliwa na kuoata mbolea ya ruzuku wakulima watakua wameifanikisha azma ya Serikali, ya kukifanya Kilimo kiwe biashara na sio adhabu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Joel Laurent alisema kuwa TFRA inafanya kampeni ya Kilimo ni mbolea katika maeneo tofauti nchini ili kutoa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea na kuhamasisha wakulima kujisajili kwenye daftari la wakulima ili wanufaike na mbolea za ruzuku.

You Might Also Like

Maadhimisho Ya VETA Ya Miaka 30 Kuhitimishwa Machi 18 Hadi 21, DSM

DIT kudhibiti nzi wa maembe kisasa

Kamati Ya Bunge Yapongeza Usimikaji Mfumo Wa Kidijitali CMA

Profesa Mutembei apongeza serikali kuruhusu mchepuo lugha ya kichina

Serikali imejipanga Mkakati wa Taifa wa Matumìzi ya nishati safi ya kupikia – Mramba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ridhiwani akutana na Mtendaji Mkuu ATE
Next Article TUGHE, DMF wateta na Ridhiwan Kikwete
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?