MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Habari

Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: TEKNOLOJIA mpya inayotumia mashine ya kuchochea mafunzo ya uchomeleaji imeleta mapinduzi makubwa katika mbinu za kufundishia uchomeleaji kwa wanafunzi wa vyuo vya ufundi nchini.

Mkufunzi kutoka Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma (VETA) Dodoma,
Manfred Mapunda amesema hayo katika maonesho ya 49 ya Kumataifa ya Biashara yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Amesema awali walikuwa wakifundisha wanafunzi kwa kutumia vifaa halisi moja kwa moja, jambo lililosababisha upotevu mkubwa wa malighafi kutokana na makosa ya mara kwa mara ya wanafunzi wakati wa mazoezi ya uchomeleaji.

“Mwanafunzi alipokosea, alilazimika kutumia vifaa vingine tena na tena, na hivyo kufanya chuo kupoteza vyuma vingi na kugharimu fedha nyingi,” amesema.

Amesema teknolojia hiyo mpya imesaidia kupunguza gharama na upotevu wa vifaa kwa kiasi kikubwa.

“Mashine hii huwapa wanafunzi nafasi ya kujifunza kwa njia ya majaribio ya kielektroniki, ambapo wanaweza kurudia mazoezi mara nyingi bila kutumia vyuma halisi.

“Mwanafunzi anaweza kurudia zoezi zaidi ya mara 10 hadi afanikiwe, bila kuchoma au kukata vyuma halisi,” amesema.

Ameongeza kuwa mbali na kupunguza gharama, teknolojia hiyo imesaidia kuongeza ufanisi katika ufundishaji.

Amesema awali idadi ya wanafunzi darasani ilipaswa isiwe zaidi ya 25 ili mwalimu aweze kuwafundisha kwa ufanisi. Lakini kupitia mfumo wa kuonyesha picha kwa kutumia projjekta sasa mwalimu anaweza kufundisha hadi wanafunzi 50 kwa wakati mmoja, huku kila mmoja akiwa na uwezo wa kuona kinachofanyika moja kwa moja ukutani.

Amesema teknolojia hiyo pia imeongeza hamasa miongoni mwa vijana, hususan wanafunzi wa kike, kushiriki katika fani ya uchomeleaji.

“Inawapa wanafunzi ujasiri na kujiamini katika kazi hii, ambayo si tu inatoa ajira bali pia kipato na fursa ya kuajiri wengine,” amesema.

Serikali kupitia VETA imeamua kuwekeza katika mashine hizo ili kusaidia katika uboreshaji wa elimu ya ufundi, kuongeza tija na kuandaa vijana kwa soko la ajira la sasa na la baadaye.

You Might Also Like

Rais Samia Awatega Wateule Wake

Mongela Ajiridhisha Ushindi wa Kishindo , Uchaguzi Serikali za Mitaa,Uchaguzi Mkuu CCM

Mpogolo Aipongeza Halmashauri Maandalizi Mikopo Asilimia 10

VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani

Makalla aitaka Halmashauri Longido kutenga fedha, ujenzi wa uzio Samia Girls

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria
Next Article Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?